BREAKINGNEWS..............BWENI LA WASICHANA CHUO CHA MKWAWA LATEKETEA KWA MOTO

Kikosi cha Zimamoto na polisi wwakizima moto katika bweni la wasichana chuo cha Mkwawa mchana huu
Chumba cha wasichana katika chuo cha mkwawa kikiwaka moto Hivi ndivyo moto ulivyoteketeza vyumba viwili katika bweni la wasichana chuo cha Mkwawa
Hapa ndipo moto ulipoanzia katika bweni hilo
Chumba ambacho moto ulianza kuwaka kikiwa kimeteketea vibaya
Mali za wanafunzi zikiwa zimeteketea kwa moto
Polisi wakichukua maelezo kwa wahanga wa tukio hilo
Mmoja kati ya wahanga akiangua kilio baada ya kufika eneo la tukio na kukuta mali zake zimeteketea kwa moto




z

m









Moto mkubwa ambao chanzo chake bado kufahamika umeteketeza vyumba viwili vya bweni la wasichana maarufu kama Hall 6 vyumba Block W katika chuo kikuu kishiriki cha elimu Mkwawa (MUCE) Iringa .

Mashuhuda wa tukio hilo wameueleza mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com kuwa chanzo cha moto huo bado hakifahamiki .

Walisema kuwa moto huo ulianza kuwaka katika chumba kimoja wapo chumba Block W muda wa saa 6 mchana na kuwa wakati huo baadhi ya wanafunzi walikuwa wamejipumzisha katika vyumba hivyo .

Hivyo walisema kuwa waliona moto huo ukianza kuwaka katika chumba kimoja wapo na kuanza jitihada za kujaribu kuzima moto huo bila mafanikio hadi kikosi cha zimatomo kutoka Manispaa ya Iringa na jeshi la polisi walipofika kuzima moto huo.

Mkuu wa chuo hicho cha Mkwawa Prof. Philimon Mushi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo la moto japo amesema kwa sasa ni mapema sana kuelezea kwa kina suala hilo na kuwa taarifa zaidi ataitoa baada ya uchunguzi wa tukio hilo kufahamika ikiwa ni pamoja na kujua madhara yaliyojitokeza na chanzo cha moto huo.

Uchunguzi wa mtandao huu umebaini kuwa moto huo umeanza kuwaka katika moja kati ya soketi za umeme katika chumba hicho hali inayoonyesha kuwa yawezekana watumiaji wa chumba hicho walikuwa wakitumia hita ama pasiChanzo; Blog ya Francis Godwin

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*