Chama cha ANC chamtimua Malema

Kiongozi wa mrengo wa vijana katika chama tawala cha ANC nchini Africa Kusini, Julius Malema, sasa ametimuliwa rasmi kutoka chama cha ANC baada ya rufaa ya kupinga uamuzi wa kutimuliwa kwake hapo awali, kutupiliwa mbali.
Kamati ya nidhamu ya chama cha ANC ilitoa uamuzi huo baada ya kusikiliza rufaa iliyowasilishwa na Malema dhidi ya kutimuliwa kwake chamani kwa kipindi cha miaka mitano kwa makosa ya kuleta mgawanyiko katika ANC.
Kamati hiyo ikiongozwa na kiongozi mkongwe na mfanyibishara Cyril Ramaphosa, iliangalia tena rufaa aliyokata Bw Malema na bado ikampata na makosa ya kukigawanya chama cha ANC pamoja na kukitia aibu.
Hata hivyo, Malema katika siku za awali ameelezea wazi kwamba atakata rufaa iwapo kamati hiyo itamsimamisha kujihusisha na shughuli za chama tawala cha ANC.
Bw Malema bado anaweza kukata rufaa katika kipindi cha miaka 14.
Julius Malema amekuwa akisisitiza kuwa anaonewa kwa sababu anataka chama hicho kutaifisha migodi ya nchi hiyo.
Pia anasema baadhi ya watu katika chama cha ANC hawamtaki kwa sababu anataka chama hicho kupata kiongozi mpya katika mkutano wake baadaye mwaka huu ili kuchukua nafasi ya Rais Jacob Zuma kuondoka

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*