Friday, March 16, 2012
KAMPENI ARUMERU: SIOI ACHANGAMKIWA NA WANANCHI WALIOFURIKA MKUTANONI KATA YA MAKIBA
Sioi akiomba kura kwa wananchi katika mkutano huo. Kushoto ni Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka na kulia ni Mratibu wa kampeni za CCM kitaifa, Katibu wa NEC, Uchumi na Fedha Mwigulu Nchemba.
Mama wa Kizanzibari, Katibu wa NEC Oganaizesheni CCM, Asha Abdallah Juma aka Mshua akisalimia wananchi katika mkutano huo
KIBAJAJI NA STAILI YA JOGOO! "Chadema sera zao za uongo kama jogoo...akiwa na jike anadanganya nitakununulia kanzu ndeeeefu hadi miguuni, lakini jogoo mwenyewe akiinama hana hata nguo ya ndani", Mbunge wa Mtera Joseph Lusinde aka Kibajaji akisema hivyo huku akionyesha kwa vitendo kwenye mkutano huo wa Makiba.
Jenerali Mstaafu, Sarakikya akimuombea kura Sioi kwenye mkutano huo. Alipanda jukwaani kwa niaba ya wazee wa Kata ya Makiba.
Msanii maarufu Hafsa Kazinja akifanya manjonjo yake kuwaburudisha wanancji wakati wa mkutano huo
"CCM DOLE TUUUU" ni maneno ya shabiki huyu wa CCM aliyokuwa akiyatoa mara kwa mara anapokunwa na hotuba za viongozi kwenye mkutano huo Kata ya Makiba
Sehemu ya maelfu ya wananchi waliofurika mkutanoni Kata ya Makiba
Mwigulu akihutubia kadamnasi
Comments