JK AMTEUA DK. RUTASITARA NAIBU KATIBU MTENDAJI 'MARCO' TUME YA MIPANGO
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com Fax: 255-22-2113425 | PRESIDENT’S OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Dkt. Longinus Kyaruzi Rutasitara kuwa Naibu Katibu Mtendaji (MARCO) Tume ya Mipango.
Taarifa iliyotolewa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Bwana Peniel Lyimo leo, Ijumaa, Februari 2, 2012, Ikulu, Dar es Salaam imesema kuwa uteuzi huo ulianza tokea Februari 20, mwaka huu wa 2012.
Kabla ya uteuzi wake, Dkt. Rutasitara alikuwa Mhadhiri Mwandamizi katika Idara ya Uchumi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
Comments