Kikosi cha jeshi kilichoundwa na Umoja wa Afrika, AU, kumsaka kiongozi wa vita vya Uganda, Joseph Kony, kinaanza kazi leo.
Kikosi hicho, chenye askari 5000, kinazinduliwa Sudan Kusini.
AU inasema kikosi kitakuwepo hadi Bwana Kony akamatwe au auwawe.
Kundi la Kony la Lord's Resistance Army, LRA, linashutumiwa kuhusika na ubakaji, mateso, mauaji na kuwalazimisha watoto kupigana vitani.
Mjumbe wa Umoja wa Mataifa katika eneo hilo, Abou Moussa, alisema inaaminiwa kuwa Bwana Kony yuko katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Bwana Moussa alisema LRA si kubwa kama ilivokuwa, lakini bado inaleta mtafaruku.
Kumetolewa wito kuwa ndege na zana za Marekani zitumiwe kuwasaka LRA
Comments