MKUTANO WA CCM KATIKA MJI MDOGO WA USA RIVER WAITIA KIHORO CHADEMA

*Yalazimika kuufanyia doria kwa helkopta na baadaye kuzusha maandamano ya pikipiki na fuso zao mitaani wakiimba 'peoples power yao' kufariji mashabiki wake.
Mgombea wa CCM Sioi  akisalimia maelfu ya watu kwenye mkutano huo
Mkutano wa CCM wa kampeni iliofanya leo jioni, umeonekana kuwatia kiwewe CHADEMA ambapo wamelazimika kuufanyia doria kwa helkopta na kama haitoshi ikabidhi wafanye maandamano ya pikipiki na fuso zao moitaani kuwafariki mashabiki wake ambao walijikunyata baada ya kishindo cha mkutano huo wa CCM uliofanyika kwenye Uwanja wa mpira wa Ngarasero na kuhudhuriwa na maelfu ya watu.

Mkutano huo ulipata wananchi wengi baada ya kuhudhuriwa hata na wananchi wa kawaida ukiachilia mbali wana-CCM waliokuwa wamejipambanua kwa kuvaa sare za chama kama Tshits, kofia au vitambaa.

Kutokana na wingi wa watu eneo la kusakatia kambumbu la uwanja huo lilifurika hadi watu wengine kuwa nje kabisa ya uwanja.

Katika hali inayoonyesha kwamba kulikuwa na mawasiliano na kati ya viongozi wa CHADEMA waliokuwa wakifanya kampeni kwa helkopta na watu waliokuwa pembeni mwa mkutano huo, baada ya mgombea wa CCM Sioi Sumari kupanda jukwaani, kiasi cha dakika mbili hivi helkopta ya CHADEMA ilipita eneo la mkutano kujaribu kushawishi watu waishangilie.

Lakini kutokana na mvuto mkubwa uliokuwa kwenye mkutano huo wengi waliendelea kumshangilia mgombea wa CCM, huku watu kadhaa waliokuwa pembeni wakijaribu kushangilia helkopta hiyo.

"Tunatisha. Hao wamepantwa presha waliposikia kwamba uwanja huu walimokuwa juzi, sisi tumefunika ndiyo maana imebidi sijui ni Mbowe au Slaa waje kujionea wenyewe" alisema Mratibu wa kampeni za CCM Mwigulu Nchemba baada ya helkopta hiyo kupita.

Juzi CHADEMA walipofanya mkutano kwenye Uwanja huo, ingawa walipata watu, lakini hawakuweza kufikisha idadi ya wale waliohudhuria mkutano wa leo wa CCM. 
Mgombea wa CCM Sioi Sumari akiwapungia mikono wananchi alipowasili kwenye mkutano huo. Mbele yake (kushoto) ni Mbunge wa Mtera Livingstone Lusinde

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.