UWAZI NA USHIRIKISHWAJI SILAHA YA MAHUSIANO BORA KAZINI

Mkurugenzi Mkuu wa TCAA Fadhili Manongi (kulia) na Mwanasheria wa TCAA Valley Chamullungu wakisaini mkataba mpya wa ushirikishwaji wa wafanyakazi kupitia Baraza la wafanyakazi na Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) Machi 26,2012 katika Ukumbi wa Mkutano wa TCAA jijini Dar es Salaam , (PIcha na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO).
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) , tawi la TCAA Bw, Eugine Lwala (kulia) na Katibu wake Matola Miti wakisaini mkataba mpya wa ushirikishwaji wa wafanyakazi Machi 26.2012 kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya TCAA jijini Dar es Salaam.(Picha na Mwanakombo Jumaa- MAELEZO).
Washiriki wa mkutano wakifuatilia kwa makini kikao.
Picha ya pamoja kati ya uongozi wa TUGHE na TCAA.
NA MAGRETH KINABO – MAELEZO
Uwazi, na ushirikishawaji hupunguza migogoro kazini.
IMEELEZWA kuwa uendeshaji wa taasisi kwa uwazi , usikivu wa viongozi na uongozi wa pamoja kati ya menejimenti na wafanyakazi katika kupanga mipango na kuweka maamuzi mbalimbali ndio nguzo kuu ya uboreshaji wa mahusiano mahali pa kazi.
Hayo yalisemwa leo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Anga Tanzania(TCAA) ,Fadhili Manongi wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi mara baada ya kutia saini mkataba mpya wa Ushirikishaji wa Wafanyakazi na Baraza la Wafanyakazi na Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya(TUGHE) na mamlaka hiyo.
Utiaji saini wa mkataba huo wa miaka mitatu ulifanyika katika ofisi za makao makuu ya mamlaka hiyo ambapo viongozi mbalimbali wa pande zote hizo walisaini. Miongoni mwa viongozi waliotia saini makataba huo ni Manongi, Katibu Mkuu Msaidizi Taifa(TUGHE), John Sanjo na Katibu wa TUGHE Mkoa wa Dares Salaam, Gaudensi Kadyanga.
“Hakuna matatizo katika tawi letu pale inapotoekea tofauti tunakaa chini tunaelezana.hivyo ni vizuri kwa viongozi mahali pa kazi kuwa wasikivu wa mambo mbalimbali kutoka kwa wafanyakazi kwa kuwa wao ndio wanaojua mambo mengi kuliko sisi tunavyojua.
“Hivyo kuna umuhimu wa kuwashirikisha wafanyakazi mambo mbalimbali na bajeti kwa kuwa wanaweza kuishauri menejimenti ili kuweza kupunguza athari zitakazoweza kujitokeza,” alisema Manongi.
Aliongeza kuwa pia yanapotoea mafanikio mahali pa kazi ni vizuri kutoa maotisha kwa wafanyakazi ili kupunguza migogoro na uchangia kuongeza ari ya kufanya kazi.
Naye Mwenyekiti wa Tawi la TUGHE la mamlaka hiyo, ambaye pia alitia saini mkataba huo, Eugene Lwala alisema mamlaka hiyo imefanikiwa kuboresha mahusiano hayo kutokana kuwa viongozi wa pande hizo zote mbili kuheshimu mipaka yao ya kazi , kuvumiliana na vikao vya mara kwa mara.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA