Asamoah and Dede Ayew nje

Mshambulizi matata Asamoah Gyan hayuko kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Ghana kilichotajwa na Kocha Kwesi Appia.
Asamoah Gyana na Dede Ayew wote nje
Gyan ameachwa nje hata baada ya shinikizo kwamba ajumuishwe kwenye kikosi cha Ghana.

Wengine waliotemwa ni mwamba wa Chelsea Michael Essien na Andre 'Dede' Ayew ambaye ana jeraha.
John Paintsil na aliyekuwa nahodha wa Ghana John Mensah nao pia hawamo.

katiuka kikosi chake kipya kocha Appiah amewajumuisha wachezaji sita wapya wengi wakiwa wanachezea soka la kulipwa ulaya. hata hivyo amejumuisha wachezaji tisa toka ligi ya nyumbani.

Asamoah Gyan aliamua kujiondoa toka timu ya taifa baada ya kushambuliwa na mashabiki baada ya uchezaji wake duni katika michuano ya kombe la bara afrika la hivi majuzi.

ilikuwa inatarajiwa kwamba angelirejea katika timu kabla ya mwezi ya Juni.
kwa upande wa Ayew , alifanyiwa upasuaji hivi majuzi nae Essien alisema atashughulika zaidi na timu yake ya Chelsea.

Kikosi cha Ghana:

Golkipa: Adam Kwarasey (Stromsgodset, Norway), Robert Dabuo (Wa All Stars), Daniel Adjei (Liberty Professionals), Ernest Sowah (Berekum Chelsea)
Walinzi: Samuel Inkoom (Dnipro, Ukraine), Daniel Opare (Standard Liege, Belgium), Harrison Afful (Esperance, Tunisia), Richard Kissi Boateng (Berekum Cheslea), Masawudu Alhassan (Genoa, Italy), John Boye (Rennes, France), Lee Addy (Dalian Aerbin, China), Daniel Addo (Arsenal Kyiv, Ukraine) Rashid Sumaila (Dwarfs), Jerry Akaminko (Manisaspor, Turkey), Isaac Vorsah (Hoffenheim, Germany)
Viungo: Anthony Annan (Vitesse Arnhem, Netherlands), Derek Boateng (Dnipro, Ukraine), Emmanuel Agyemang Badu (Udinese ,Italy), Rabiu Mohammed (Evian, France) Richard Mpong (Medema) Albert Adomah (Bristol City, England), Christian Atsu (Rio Ave, Portugal), Ishamel Yartey, (Servette, Switzerland), Sulley Muntari (AC Milan, Italy), Kwadwo Asamoah (Udinese, Italy).
Washambulizi: Jordan Ayew (Marseille, France), Dominic Adiyiah (Arsenal Kyiv, Ukraine), Ben Acheampong (Kotoko), Emmanuel Baffour (New Edubiase), Emmanuel Clottey (Berekum Chelsea).

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.