MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA CHUO KIPYA CHA UFUNDI STADI VETA CHA MKOA WA MANYARA
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib
Bilal, na Balozi wa Korea Kusini, Young Hoon Kim, kwa pamoja wakikata
utepe kuzindua rasmi chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi cha VETA
kilichojengwa Wilaya ya Babati Mkoani Manyara, wakati wa hafla ya
ufunguzi wa chuo hicho iliyofanyika jana Aprili 30, 2012, mkoani
Manyara. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed
Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja kwa kumbukumbu na viongozi wa
Chuo cha Veta na viongozi wa Serikali baada ya ufunguzi rasmi wa chuo
hicho uliofanyika jana Aprili 30, 2012 mkoani Manyara. Picha na Muhidin
Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano:- wa Tanzania, Dkt. Mohammed
Gharib Bilal, akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo la Chuo kipya cha
VETA, baada ya kufungua rasmi chuo hicho kilichojengwa Wilaya ya Babati
mkoa wa Manyara. Hafla ya ufunguzi wa Chuo hicho ilifanyika jana Aprili
30, 2012, mkoani Manyara. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib
Bilal, akimsikiliza maelezo kutoka kwa Mwalimu wa ufundi wa Magari wa
Chuo kipya cha VETA cha Mkoani Manyara, Treekta dogo linalotumika
kulimia na kupandia Mbegu za mazao, wakati aliokuwa akitembelea na
kukagua majengo mapya ya Karakana ya chuo hicho baada ya kukifungua
rasmi jana Aprili 30, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Comments