Mama Kikwete awataka wanawake kutokutoa mimba
Na Anna Nkinda – Maelezo, Mbeya
Wanawake nchini wametakiwa kutokuwatupa watoto wanaowazaa hata kama wanakabiliwa na changamoto za kimaisha za kushindwa kuwalea kwani kwa kufanya hivyo wanamkosea Mwenyezi Mungu pia hawawezi jua watoto hao watakuwa na hali gani ya kimaisha kwa siku za baadaye.
Wito huo umetolewa jana na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati akiongea na wanawake waliohudhuria sherehe za siku ya mwanamke wa Chuo Kikuu Cha Teofilo Kisanji (TEKU) kilichopo jijini Mbeya.
Aidha Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) alisema kuwa usawa wa kijinsia katika elimu na fursa za kiuchumi zimeendelea kuwa changamoto kwa wanawake Duniani kote hata hivyo hatua kubwa imefikiwa ya kuwakomboa wanawake wengi kutoka lindi la umasikini.
“Tunatambua kwamba wanawake wanaposhiriki kikamilifu katika shughuli za jamii uchumi wa nchi hukua zaidi. Hivyo siku kama ya leo ni nyenzo muhimu katika kuwawezesha wanawake kujifunza kutoka kwa wengine jinsi walivyofanikiwa , kubadilishana uzoefu na kuelimishana. Kwani elimu yenye manufaa ni ile inayolenga kuwakomboa watu kutokana na changamoto zinazowakabili”, alisema Mama Kikwete.
Comments