May 15
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akikabidhi kombe la ushindi la “Jihadi Cup” kwa kepteni wa timu ya Sayari iliyoibuka kidedea kwenye ligi hiyo iliyozishirikisha timu 9 za daraja la pili na tatu kwa wilaya ya mjini.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akikagua timu ya Taifa Jipya iliyoingia kwenye finali za Jihadi Cup, huko uwanja wa Amaan Mjini Zanzibar. Taifa Jipya ilishindwa na wapinzani wao timu ya Sayari kwa mikwaju ya penalty (5-3).
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akikagua timu ya Sayari iliyoingia kwenye finali za “Jihadi Cup”, huko uwanja wa Amaan Mjini Zanzibar. Sayari ilinyakuwa ubingwa kwa kuwashinda wapinzani wao timu ya Taifa Jipya kwa mikwaju ya penalty (5-3).
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akiwa katika picha ya pamoja na Mwakilishi wa Jimbo la Magogoni Mheshimiwa Abdillahi Jihadi Hassan (kushotoni kwake), pamoja na baadhi ya viongozi wa ZFA na kamati ya michezo ya “Jihadi Cup”.Picha na Salmin Said-Ofisi Ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
Comments