|
Maofisa wa kampuni ya Superdoll, Jamal Bayser kulia na Ibrahim Juma kushoto wakisubiri mechi hiyo. |
MECHI ya mwisho ya mashindano ya Afrika ya Netiboli yanayofikia tamati leo Dar es Salaam, kati ya wenyeji Tanzania na Botswana imechelewa kuanza kutokana na mvua inayoendelea kwenye Uwanja wa Taifa.
Mgeni rasmi, mke wa makamu wa rais, mama Bilal na mke wa Waziri Mkuu mama Pinda hawajafika bado. Tayari CHANETA imeamua mechi zihamie Uwanja wa ndani wa Taifa.
Mechi hiyo ilipangwa kuanza saa 7:00 mchana na Tanzania ikishinda itakuwa mshindi wa pili, wakati Malawi tayari wametetea ubingwa wao kwa kushinda mechi zote. Na Bin Zubery Blog
|
Gwiji wa mpira wa kikapu Tanzania Saleh Zonga kulia |
|
Wachezaji na maofisa wa Zambia |
|
Wachezaji wa mabingwa wa Afrika Netoboli, Malawi |
Comments