OFISI YA MKUU WA MKOA RUKWA YATEKELEZA AGIZO LA OFISI YA MAKAMU WA RAIS KWA KUTENGA SIKU MAALUM YA USAFI WA MAZINGIRA LEO

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akifyeka maua kuyaweka sawa katika moja ya bustani katika Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huyo leo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Ofisi ya Makamu wa Rais inayozitaka taasisi za Umma na Serikali kuwa na siku maalum ya usafi wa mazingira katika maeneo yao. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa imejiwekea utaratibu wa kufanya usafi kila siku ya alhamisi ya wiki ambapo kila mtumishi anashiriki katika jukumu hilo. Usafi huo huanza saa mbili hadi saa tatu asubuhi. Miongoni mwa kazi zinazofanyika ni pamoja kufagia, kufyeka, uzoaji wa taka ngumu, na usafi wa jumla katika jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.
 Zoezi la usafi likiwa linaendelea
Kutoka kushoto ni Afisa Elimu Taalum Mkoa Domician Chose na Kaimu Katibu wa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Frank Jailos Mateny wakijumuika kwenye usafi huo leo.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa akipeana neno la mwisho na watumishi wake mara baada ya zoezi hilo la usafi kukamilika.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

GSM ARIDHIA UJENZI WA UWANJA WA YANGA JANGWANI

WACHEZAJI YANGA WAGOMA KABISA KUFANYA MAZOEZI LEO, LWANDAMINA AIBUKA PEKE YAKE SHAMBA LA BIBI

DKT. MAJULE AMFANYIA MAPOKEZI MAKUBWA BALOZI WA CHINA NCHINI

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

Wasifu wa Kizza Besigye

HERSI KWENDA KUSOMA TENA CHUO KIKUU CHA OXFORD UINGEREZA