Serikali Yapiga Marufuku Mikusanyiko Yote isiyokuwa na Kibali

Na Juma Mohammed,MAELEZO

Zanzibar Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imepiga marufuku mikusanyiko ya aina yoyote ikiwemo mihadhara ya aina mbalimbali ambayo hajapata kibali cha Serikali.

 Akitoa taarifa ya Serikali,Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais ,Mohammed Aboud Mohammed amesema mbali na suala hilo,pia imewataka wananchi kuheshimu sheria.

 Waziri Aboud amesema pia Serikali imeliagiza Jeshi la Polisi kuwatafuta na kuwafikisha katika vyombo vya sheria wale wote waliohusika na fujo zilizotokea jana na leo katika mji wa Zanzibar. “Serikali inakemea vikali vitendo vyote vya hujuma na uharibifu wa mali zilizofanywa katika taasisi za umma,Dini na watu binafsi” Alisisitiza Waziri huyo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

GSM ARIDHIA UJENZI WA UWANJA WA YANGA JANGWANI

WACHEZAJI YANGA WAGOMA KABISA KUFANYA MAZOEZI LEO, LWANDAMINA AIBUKA PEKE YAKE SHAMBA LA BIBI

DKT. MAJULE AMFANYIA MAPOKEZI MAKUBWA BALOZI WA CHINA NCHINI

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

Wasifu wa Kizza Besigye

HERSI KWENDA KUSOMA TENA CHUO KIKUU CHA OXFORD UINGEREZA