TFF yaikodolea macho Super Sport

SHIRIKISHO la Soka Tanzania, TFF, liko katika mchakato wa mazungumzo na kituo cha SuperSport cha Afrika Kusini kwa ajili ya kuonyesha mechi zake za Ligi Kuu msimu ujao.

Wakati TFF ikijipanga kufanya hivyo, kituo hicho tayari kinafanya hivyo kwa Ligi Kuu ya Kenya na Uganda.

Itakumbukwa, Super Sport ilikuwa ikionyesha baadhi ya mechi za Ligi Kuu Bara na zaidi ni zile zinazohusisha timu za Simba na Yanga na kuonekana sehemu mbalimbali duniani.

Mwenyekiti wa Kamati ya Ligi, Walas Karia alisema katika mazungumzo ya kwanza pande hizo mbili zilishindwa kufikia makubaliano na baada ya Super Sport kutoa  kupendekeza yake kuwa baadhi ya mambo lazima yafanyike iweze kudhamini ligi hiyo.

"Kwa sasa kamati ipo katika harakati kukutana na viongozi wa Super Sport kuhakikisha Ligi Kuu msimu ujao inakuwa ya kuvutia ikiwemo pia kutafuta wadhamini mbalimbali lengo likiwa kupunguza makali ya gharama za uendeshaji kwa klabu."


Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA