IDARA ya Afya wilayani Muheza, imevifunga vibanda vya kuuza nyama choma ya nguruwe (pichani) kutokana na ugonjwa wa kipindupindu ambao unatikisa wilayani hapa.
Vibanda hivyo vilifungwa juzi na maofisa afya wa Wilaya ya Muheza, chini ya ulinzi wa polisi. Akizungumzia suala hilo, Mratibu wa Shughuli za Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) wilayani Muheza, Boniface Jacob alisema wameamua kufunga vibanda hivyo kutokana na mazingira machafu ambayo yanaweza kuchochea mlipuko wa kipindupindu.
Jacob alisema vibanda hivyo havifai kwa biashara ya chakula cha binadamu na kwamba, havijasajiliwa na TFDA. Alisema hakuna machinjio ya nguruwe wilayani Muheza na kwamba, nyama hiyo haikaguliwi na mkaguzi wa nyama wa wilaya. Mratibu huyo alisema kuwa kutokana na hali hiyo, nyama hiyo ya nguruwe siyo salama kwa binadamu.
Alisema mbali ya kipindupindu walaji pia wanaweza kuambukizwa magonjwa kama mafua ya nguruwe, minyoo na magonjwa mengine hatari. Jacob alisema vibanda hivyo vimefungwa mpaka hapo sheria na taratibu za biashara ya chakula cha binadamu zitakapofuatwa.
Wakati huohuo,watumiaji wa kilaji hicho cha nyama ya nguruwe wameonekana kuhaha kutokana na vibanda vinavyouza nyama hiyo kufungwa. e&p
Vibanda hivyo vilifungwa juzi na maofisa afya wa Wilaya ya Muheza, chini ya ulinzi wa polisi. Akizungumzia suala hilo, Mratibu wa Shughuli za Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) wilayani Muheza, Boniface Jacob alisema wameamua kufunga vibanda hivyo kutokana na mazingira machafu ambayo yanaweza kuchochea mlipuko wa kipindupindu.
Jacob alisema vibanda hivyo havifai kwa biashara ya chakula cha binadamu na kwamba, havijasajiliwa na TFDA. Alisema hakuna machinjio ya nguruwe wilayani Muheza na kwamba, nyama hiyo haikaguliwi na mkaguzi wa nyama wa wilaya. Mratibu huyo alisema kuwa kutokana na hali hiyo, nyama hiyo ya nguruwe siyo salama kwa binadamu.
Alisema mbali ya kipindupindu walaji pia wanaweza kuambukizwa magonjwa kama mafua ya nguruwe, minyoo na magonjwa mengine hatari. Jacob alisema vibanda hivyo vimefungwa mpaka hapo sheria na taratibu za biashara ya chakula cha binadamu zitakapofuatwa.
Wakati huohuo,watumiaji wa kilaji hicho cha nyama ya nguruwe wameonekana kuhaha kutokana na vibanda vinavyouza nyama hiyo kufungwa. e&p
Comments