KIGOMA ALL STARS KWA KUSHIRIKIANA NA MBUNGE WAO ZITTO KABWE WANATARAJIA KUFUNGUA CENTRE YA VIJANA KIGOMA

LEKA DUTIGITE KIGOMA.. ni tamasha kubwa linalotarajiwa kufanyika mkoani Kigoma  tarehe 17 ndani ya mwezi huu wa saba na kuwashwa moto na wasanii  wazawa wa kigoma. Mpaka sasa ari waliyonayo wasanii  hao ni ya kubwa mno.. mpaka imekuwa kama ni changamoto kwa wasanii wanaotoka katika mikoa mingine, na kulowea zaidi Dar es Salaam.

Hata hivyo breaking news inaonyesha kuwa karibia nusu ya nyimbo zinazofanya vizuri hivi  sasa katika soko la muziki hapa nchini ni za wasanii wanaotoka katika mkoa wa kigoma. Angalia nyimbo kama "Kichwa kinauma" yake Ali Kiba aliyomshirikisha Jaydee, "Upepo" Recho, "Mawazo" Diamond, "Maneno maneno" Queen Darleen, "Jua ni wewe" Mwasiti akimshirikisha Ally Nipishe, Na nyingine nyingi kutoka kwa wasanii wao kina Chege, Abdu Kiba, Baba Levo, Makomandoo Bongo, Linex, Banana Zorro na wengine wengi.
Jambo lingine la kutia hamasa ni jinsi Mbunge wao wa Kigoma Zitto Kabwe anavyoshirikiana nao katika kila jambo. Naye msimamizi wa ama mratibu wa tamasha hilo Mwasiti Almas naye alifunguka na kusema haya "Kila kitu kwetu kama wasanii wa Kigoma kiko tayari kwa ajili ya tamasha hili, Kilichobaki ni wasanii wenyewe kufika mkoani kwao na kutimiza lengo la Tamasha hili, kwani tamasha hili linasimama kuwatia chachu ama hamasa vijana wa mkoa wa Kigoma mkoani humo".

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU