MTAKATIFU THOM ASAINI MIAKA MIWILI YANGA, ASEMA HAKUJA KULA BATA, AMEKUJA KUPIGA KAZI

Kocha mpya wa Yanga, Thom Saintfiet jioni hii amesaini mkataba wa miaka miwili wa kuifundisha klabu hiyo na baada ya kusaini, akasema hakuja Tanzania ‘kustarehe’ amekuja kufanya kazi na sera yake ni ushindi. Anataka ushindi na mataji. Amesema jaribio lake la kwanza ni kutetea ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, katika michuano inayoanza Julai 14, Dare s Salaam (Habari kamili baadaye). Tazama picha za kusaini kwake Mkataba makao makuu ya klabu, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam. (PICHA ZOTE KWA HISANI YA BIN ZUBEIRY BLOG
Kulia ni Katibu wa Yanga, Celestine Mwesigwa, katikati Thom anasaini. Kushoto The Don Seif Ahmad 'Magari'


Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA