MWANDISHI MWANDAMIZI WA MICHEZO AFARIKI DUNIA

Mwandishi Mwandamizi wa Habari za Michezo, Chris Mwambonda amefariki usiku wa kuamkia leo jijini Dar es Salaam kwa mujibu wa rafiki wa karibu wa Marehemu Mwambonda, Mawazo Lusonzo.  

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Mwananyamala na mipango ya maziko inafanyika nyumbani kwa mama yake mzazi Goba na mipango ya mazishi inafanyika huko huko, taarifa zaidi zitatolewa baadaye. 

Pichani ni moja katika ya matukio aliyoshiriki enzi za uhai wake ambapo hapa anaonekana akikabidhiwa cheti cha ushiriki wa mafunzo yaliyowashirikisha wahariri wa michezo na Mkurugenzi wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Leonard Thadeo baada ya semina ya wahariri wa michezo iliyofanyika Juni 10 2010. 


Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, Ameni.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI