NHIF Nyanda za Juu kutumia Takukuru

MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, umesema utatumia Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), ili kubaini halmashauri ambazo zinafuja fedha zake.

Akizungumza mjini hapa, Meneja wa kanda, Celestin Mganga, alisema kuna mchezo mchafu unaofanywa kwa baadhi ya halmashauri kuandika hundi nyingi kwa malengo la kukomoa mfuko na kwamba, hawatavumilia hali hiyo na watahakikisha wanafuatilia kwa umakini.

“Hatutoweza kuvumia mchezo huo, lazima sasa tutumie Takukuru ili kudhibiti hali hiyo, kwani ina lengo mabaya tunajikuta hatuna wateja wengi na wananchi kutojua maana ya mradi huo,” alisema Mganga.

Pia, Mganga aliagiza waratibu wa NHIF kutoa elimu zaidi kwa wananchi hususan vijijini kujiunga na mfuko huo, ili kuwarahisishia upatikanaji huduma za afya kwa urahisi katika zahanati na vituo vya afya.

“Kumekuwapo na changamoto nyingi hususan wananchi kutokuwa na mwamko wa kujiunga na mfuko wa bima ya afya, hivyo kuna ulazima wa waratibu kuingia vijijini zaidi ili kupata wateja wengi zaidi,” alisema. Chanzo: Gazeti la Mwananchi Julai 03.12

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI