TUTUMIE HABARI NA PICHA MDAU!!

Sunday, July 1, 2012

Dkt Harisson Mwakyembe:Serikali kuboresha viwanja vya ndege hapa nchini

Na Gladness Mushi wa Fullshangwe-Arusha

SERIKALI imesema kuwa ipo kwenye mchakato wa kuviboresha viwanja

mbalimbali vya ndege hapa nchini ukiwemo uwanja wa ndege wa Arusha kwa
kuufanyia matengenezo makubwa uweze kuruhusu kutua kwa ndege kubwa za
kimataifa.

Waziri wa uchukuzi ,Dkt Harisson Mwakyembe aliyesema hayo jana baada

ya kupokea taarifa fupi wakati akiongea na wafanyakazi wa kiwanja cha
ndege cha Arusha baada ya kufanya ziara fupi mkoani hapa.

Dkt Mwakyembe alisema kuwa uwanja wa ndege wa Arusha unaumuhimu wa

kipekee katika kuendeleza utalii wa ndani na kueleza kuwa serikali
itafanya kila njia kuhakikisha kuwa uwanja huo unapanuliwa na kuwa na
uwezo wa kutua ndege kubwa.

Alisema amekuwa akipata malalamiko mengi kuwa uwanja huo umekuwa

ukitumika kunyangánya wateja wa uwanja wa kimataifa wa
Kilimanjaro(KIA) huku maombi hayo yakitaka uwanja huo ufungwe.

‘’nimepata taarifa za kutaka kufungwa kwa  uwanja huu wa ndege wa

Arusha kwa kuwa unatumika kunyangánya abilia wa uwanja wa KIA
,nimejiridhisha kuwa kiwanja hiki kina umuhumu wa kipekee na serikali
itaangalia uwezekano wa kukiboresha’’alisema Mwakyembe.

Alisema serikali itatenga fedha zaidi  kwa ajili ya kukiboresha

kiwanja hicho ili kiwe cha kisasa zaidi ,ikiwa ni pamoja na
kuviboresha viwanja vingine vya Songwe,Kigoma na Mwanza.

Awali Kaimu mkurugenzi wa kiwanja cha ndege cha Arusha,Mhandisi

Suleiman Suleiman alisema kuwa kiwanja hicho kinakabiliwa na
changamoto nyingi ikiwemo ukosefu wa eneo la maegesho ya ndege, jengo
la abilia na jengo  la zima moto.

Alisema changamoto zingine ni pamoja na kutokuwa na taa zinazowaka

majira ya usiku hivyo kutoruhusu ndege kutua ama kuruka nyakati za
usiku,kituo cha umeme ,Mnara wa kuongozea ndege ,Jengo la hali ya hewa
,jengo la Mizigo  pamoja na miundombinu yake.

Aidha alisema kuwa ukarabati wa kiwango cha lami wa barabara ya kuruka

na kutua yenye urefu wa mita 420 uliogharimu kiasi cha shilingi
bilioni  1.7umefanya urefu wa barabara hiyo kufikia mita 1620 hivyo
kuwezesha  ndege zenye ukubwa wa kubeba abilia 70 kuweza kutua katika
kiwanja hicho.

Mhandisi Sulemeni aliongeza  kuwa kwa sasa kiwanja hicho kinahudumia

wastani ndege 1700 kwa mwaka na abilia wanaohudumia kwa mwezi ni
12,000.

Alisema kuwa mpango wa sasa ni kuhamisha barabara ya Arusha Babati na

tayari wamemweleza wakala wa barabara mkoani Arusha(Tanroads).

Aliongeza kuwa hatua hiyo itasaidia kuondoa msongamano uliopo sasa,

pamoja na kuhamisha barabara ya sasa ya kuingia kiwanjani hapo kwani
inaingiliana na maegesho.

MANAHODHA STARS WANG’ARA TUZO ZA VODACOM


Nahodha wa Taifa Stars, Juma Kaseja na msaidizi wake Aggrey Morris wameng’ara katika hafla ya kampuni ya Vodacom kukabidhi zawadi kwa wachezaji, klabu, waamuzi na makocha waliofanya vizuri kwenye Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2011/2012. 
Katika hafla hiyo iliyofanyika jana usiku (Juni 30 mwaka huu) hoteli ya Double Tree Hilton, Dar es Salaam, Morris anayechezea Azam aliibuka mchezaji bora wa ligi hiyo wakati Kaseja anayedakia Simba alikuwa kipa bora.
 
Kila mmoja alizawadiwa sh. 3,312,500 katika hafla hiyo ambayo mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye. Kaseja aliwashinda makipa Mwadili Ally (Azam) na Deogratias Munishi (Mtibwa Sugar) wakati Morris aliwashinda Haruna Niyonzima (Yanga) na Haruna Moshi (Simba).
 
John Bocco wa Azam aliyefunga mabao 19 ndiye mfungaji bora, refa bora ni Martin Saanya kutoka Morogoro ambaye aliwashinda Oden Mbaga (Dar es Salaam) na Amon Paul (Mara) wakati kocha bora ni Stewart Hall wa Azam aliyewashinda Charles Kilinda (JKT Ruvu) na Charles Mkwasa (Ruvu Shooting). Kila mshindi mepata sh. 3,875,000.
 
Timu yenye nidhamu bora ni Azam iliyopata sh. 7,750,000, mshindi wa tatu Yanga sh. 15,500,000, makamu bingwa Azam sh. 22,000,000 na bingwa Simba sh. 50,000,000.
 
Pia Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewazawadia sh. 1,000,000 kila mmoja kwa wachezaji watatu vijana wenye umri chini ya miaka 20 waliofanya vizuri kwenye ligi hiyo.
 
Wachezaji hao ambao walikuwa kwenye vikosi vya kwanza vya timu zao ni Frank Domayo (JKT Ruvu), Rashid Mandawa (Coastal Union) na Hassan Dilunga (Ruvu Shooting).

AIRTEL YAWASAIDIA WANAWAKE WA DIWA

Afisa Uhusiano na Matukio wa Airtel Dangio Kaniki (kulia) akiwakabidhi fedha taslim wanawake wa Dar Indian Women Association (DIWA) kwa ajili ya kuchangia mfuko wa kuwasaidia wanawake hao ambao wanajishughulisha na shughuli za kusaidia wanawake mbalimbali hapa nchini.

HOTUBA YA MHE. DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KWA WANANCHI, TAREHE 30 JUNI, 2012


Ndugu Wananchi,
              Kama ilivyo ada naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehma, kwa kutujaalia uzima na kutuwezesha kumaliza nusu ya kwanza ya mwaka 2012 salama.  Kwa kutumia utaratibu wetu wa kuzungumza nanyi kila mwisho wa mwezi, leo napenda kuzungumzia mambo mawili. Jambo la kwanza ni suala la usafirishaji haramu wa binadamu nchini na la pili ni la mgomo wa madaktari. 
Usafirishaji Haramu wa Binadamu Nchini
Ndugu Wananchi;
              Bila ya shaka mtakuwa mmezisikia taarifa za tukio la kushtusha na kuhuzunisha la kukutwa maiti 43 za watu wasiojulikana, zilizotupwa katika kichaka kilichopo kijiji cha Chitego, Wilayani Kongwa, Mkoa wa Dodoma tarehe 26 Juni, 2012.  Pamoja na maiti hao, walipatikana watu 84 wakiwa hai lakini wote wakiwa wamedhoofu na baadhi yao wakiwa mahututi.  Hatua za haraka zilichukuliwa kuwasafirisha watu hao hadi Dodoma ambapo wale waliokuwa mahututi walifikishwa Hospitali Kuu ya Mkoa wa Dodoma kwa matibabu na wengine walihifadhiwa katika Kituo cha Kati cha Polisi, Dodoma.  Maiti 22 zilipelekwa Dodoma na 21 zilipelekwa Morogoro kuhifadhiwa.
Taarifa zilizopatikana kutoka kwa wale walionusurika zimebainisha kuwa watu hao ni raia wa Ethiopia ambao walikuwa safarini kwenda Malawi na baadaye Afrika ya Kusini ambako wangetengenezewa utaratibu wa kwenda kuishi Marekani na Ulaya.  Kwa mujibu wa maelezo yao, safari yao ilianza miezi mitano iliyopita.  Mwezi mmoja waliutumia Ethiopia na miezi minne waliitumia Kenya kabla ya kuletwa Arusha ambako walipakiwa kwenye lori na kuanza safari ya kuelekea Malawi lakini ikaishia Chitego.  Lori walilopanda lilikuwa limezibwa kabisa na hivyo kusababisha vifo kwa kukosa hewa.
Tukio la Chitego, Dodoma la wahamiaji haramu kukamatwa na wengine kukutwa wamekufa si la kwanza kutokea hapa nchini.  Kwa jumla, katika kipindi cha takriban miaka 10 sasa kumekuwepo na tatizo kubwa la wahamiaji haramu kuingia nchini.  Kwa mfano, kati ya mwaka 2005 na hivi sasa jumla ya wahamiaji haramu 19,683 wamekamatwa.  Karibu wote wameshaondoshwa nchini na hivi sasa wapo karibu watu 1,500 tu magerezani wanaotumikia adhabu na kusubiri kurejeshwa makwao.  Wengi wa watu hao wanatoka Ethiopia na Somalia na baadhi kutoka Pakistan na Bangladesh.
Wahamiaji haramu wamekuwa wanaingia nchini kwa kupitia njia zisizo rasmi.  Wapo wanaotumia nchi kavu hasa kupitia mikoa ya Mara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga.  Na, wapo wanaopitia baharini kwa kutumia fukwe za Pemba, Unguja na za mikoa ya ukanda wa Pwani ya Tanzania Bara yaani Tanga, Pwani, Lindi na Mtwara.
Ndugu Wananchi;
Kwa mujibu wa kauli zao, watu hao wamekuwa wanaeleza kuwa hawaji nchini kuhamia bali wao ni wapita njia tu.  Wanaelekea Afrika ya Kusini ambako wameahidiwa kuwa watatengenezewa mipango ya kuhamia Marekani na Ulaya.  Watu hao pia wamethibitisha kuwepo kwa watu maalum wanaojihusisha na usafiri wao tangu nchi watokako na zote wanazopitia mpaka kule waendako.  Aidha, wamesema kuwa wao wanawalipa watu hao ili wawasafirishe na hakika si kiwango kidogo.  Kwa jumla ni kwamba hili si suala la uhamiaji haramu bali ni la biashara haramu ya kusafirisha binadamu.
Ndugu Wananchi;
Kufuatia vyombo vyetu vya usalama kuwa makini na watu wengi kukamatwa ndipo wasafirishaji walipobuni njia za kuwasafirisha kama mizigo.  Makontena, malori yaliyofunikwa nyuma na matenki ya mafuta na ya maji yamekuwa yanatumika kwa ajili hiyo.  Usafiri wa aina hiyo ndiyo uliosababisha vifo vilivyotokea Dodoma tarehe 26 Juni, 2012 na vya watu 21 vilivyotokea mwezi Desemba, 2011 Mkoani Morogoro, na vile vya watu 12 vilivyotokea katika matukio mawili ya Mkoa wa Mbeya, mwezi Mei, 2012.
Ndugu Wananchi;

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*