Sunday, July 1, 2012
Dkt Harisson Mwakyembe:Serikali kuboresha viwanja vya ndege hapa nchini
Na Gladness Mushi wa Fullshangwe-Arusha
SERIKALI imesema kuwa ipo kwenye mchakato wa kuviboresha viwanja
mbalimbali vya ndege hapa nchini ukiwemo uwanja wa ndege wa Arusha kwa
kuufanyia matengenezo makubwa uweze kuruhusu kutua kwa ndege kubwa za
kimataifa.
Waziri wa uchukuzi ,Dkt Harisson Mwakyembe aliyesema hayo jana baada
ya kupokea taarifa fupi wakati akiongea na wafanyakazi wa kiwanja cha
ndege cha Arusha baada ya kufanya ziara fupi mkoani hapa.
Dkt Mwakyembe alisema kuwa uwanja wa ndege wa Arusha unaumuhimu wa
kipekee katika kuendeleza utalii wa ndani na kueleza kuwa serikali
itafanya kila njia kuhakikisha kuwa uwanja huo unapanuliwa na kuwa na
uwezo wa kutua ndege kubwa.
Alisema amekuwa akipata malalamiko mengi kuwa uwanja huo umekuwa
ukitumika kunyangánya wateja wa uwanja wa kimataifa wa
Kilimanjaro(KIA) huku maombi hayo yakitaka uwanja huo ufungwe.
‘’nimepata taarifa za kutaka kufungwa kwa uwanja huu wa ndege wa
Arusha kwa kuwa unatumika kunyangánya abilia wa uwanja wa KIA
,nimejiridhisha kuwa kiwanja hiki kina umuhumu wa kipekee na serikali
itaangalia uwezekano wa kukiboresha’’alisema Mwakyembe.
Alisema serikali itatenga fedha zaidi kwa ajili ya kukiboresha
kiwanja hicho ili kiwe cha kisasa zaidi ,ikiwa ni pamoja na
kuviboresha viwanja vingine vya Songwe,Kigoma na Mwanza.
Awali Kaimu mkurugenzi wa kiwanja cha ndege cha Arusha,Mhandisi
Suleiman Suleiman alisema kuwa kiwanja hicho kinakabiliwa na
changamoto nyingi ikiwemo ukosefu wa eneo la maegesho ya ndege, jengo
la abilia na jengo la zima moto.
Alisema changamoto zingine ni pamoja na kutokuwa na taa zinazowaka
majira ya usiku hivyo kutoruhusu ndege kutua ama kuruka nyakati za
usiku,kituo cha umeme ,Mnara wa kuongozea ndege ,Jengo la hali ya hewa
,jengo la Mizigo pamoja na miundombinu yake.
Aidha alisema kuwa ukarabati wa kiwango cha lami wa barabara ya kuruka
na kutua yenye urefu wa mita 420 uliogharimu kiasi cha shilingi
bilioni 1.7umefanya urefu wa barabara hiyo kufikia mita 1620 hivyo
kuwezesha ndege zenye ukubwa wa kubeba abilia 70 kuweza kutua katika
kiwanja hicho.
Mhandisi Sulemeni aliongeza kuwa kwa sasa kiwanja hicho kinahudumia
wastani ndege 1700 kwa mwaka na abilia wanaohudumia kwa mwezi ni
12,000.
Alisema kuwa mpango wa sasa ni kuhamisha barabara ya Arusha Babati na
tayari wamemweleza wakala wa barabara mkoani Arusha(Tanroads).
Aliongeza kuwa hatua hiyo itasaidia kuondoa msongamano uliopo sasa,
pamoja na kuhamisha barabara ya sasa ya kuingia kiwanjani hapo kwani
inaingiliana na maegesho.
SERIKALI imesema kuwa ipo kwenye mchakato wa kuviboresha viwanja
mbalimbali vya ndege hapa nchini ukiwemo uwanja wa ndege wa Arusha kwa
kuufanyia matengenezo makubwa uweze kuruhusu kutua kwa ndege kubwa za
kimataifa.
Waziri wa uchukuzi ,Dkt Harisson Mwakyembe aliyesema hayo jana baada
ya kupokea taarifa fupi wakati akiongea na wafanyakazi wa kiwanja cha
ndege cha Arusha baada ya kufanya ziara fupi mkoani hapa.
Dkt Mwakyembe alisema kuwa uwanja wa ndege wa Arusha unaumuhimu wa
kipekee katika kuendeleza utalii wa ndani na kueleza kuwa serikali
itafanya kila njia kuhakikisha kuwa uwanja huo unapanuliwa na kuwa na
uwezo wa kutua ndege kubwa.
Alisema amekuwa akipata malalamiko mengi kuwa uwanja huo umekuwa
ukitumika kunyangánya wateja wa uwanja wa kimataifa wa
Kilimanjaro(KIA) huku maombi hayo yakitaka uwanja huo ufungwe.
‘’nimepata taarifa za kutaka kufungwa kwa uwanja huu wa ndege wa
Arusha kwa kuwa unatumika kunyangánya abilia wa uwanja wa KIA
,nimejiridhisha kuwa kiwanja hiki kina umuhumu wa kipekee na serikali
itaangalia uwezekano wa kukiboresha’’alisema Mwakyembe.
Alisema serikali itatenga fedha zaidi kwa ajili ya kukiboresha
kiwanja hicho ili kiwe cha kisasa zaidi ,ikiwa ni pamoja na
kuviboresha viwanja vingine vya Songwe,Kigoma na Mwanza.
Awali Kaimu mkurugenzi wa kiwanja cha ndege cha Arusha,Mhandisi
Suleiman Suleiman alisema kuwa kiwanja hicho kinakabiliwa na
changamoto nyingi ikiwemo ukosefu wa eneo la maegesho ya ndege, jengo
la abilia na jengo la zima moto.
Alisema changamoto zingine ni pamoja na kutokuwa na taa zinazowaka
majira ya usiku hivyo kutoruhusu ndege kutua ama kuruka nyakati za
usiku,kituo cha umeme ,Mnara wa kuongozea ndege ,Jengo la hali ya hewa
,jengo la Mizigo pamoja na miundombinu yake.
Aidha alisema kuwa ukarabati wa kiwango cha lami wa barabara ya kuruka
na kutua yenye urefu wa mita 420 uliogharimu kiasi cha shilingi
bilioni 1.7umefanya urefu wa barabara hiyo kufikia mita 1620 hivyo
kuwezesha ndege zenye ukubwa wa kubeba abilia 70 kuweza kutua katika
kiwanja hicho.
Mhandisi Sulemeni aliongeza kuwa kwa sasa kiwanja hicho kinahudumia
wastani ndege 1700 kwa mwaka na abilia wanaohudumia kwa mwezi ni
12,000.
Alisema kuwa mpango wa sasa ni kuhamisha barabara ya Arusha Babati na
tayari wamemweleza wakala wa barabara mkoani Arusha(Tanroads).
Aliongeza kuwa hatua hiyo itasaidia kuondoa msongamano uliopo sasa,
pamoja na kuhamisha barabara ya sasa ya kuingia kiwanjani hapo kwani
inaingiliana na maegesho.
MANAHODHA STARS WANG’ARA TUZO ZA VODACOM
Nahodha wa Taifa Stars, Juma Kaseja na msaidizi wake Aggrey Morris wameng’ara katika hafla ya kampuni ya Vodacom kukabidhi zawadi kwa wachezaji, klabu, waamuzi na makocha waliofanya vizuri kwenye Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2011/2012.
Katika hafla hiyo iliyofanyika jana usiku (Juni 30 mwaka huu) hoteli ya Double Tree Hilton, Dar es Salaam, Morris anayechezea Azam aliibuka mchezaji bora wa ligi hiyo wakati Kaseja anayedakia Simba alikuwa kipa bora.
Kila mmoja alizawadiwa sh. 3,312,500 katika hafla hiyo ambayo mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye. Kaseja aliwashinda makipa Mwadili Ally (Azam) na Deogratias Munishi (Mtibwa Sugar) wakati Morris aliwashinda Haruna Niyonzima (Yanga) na Haruna Moshi (Simba).
John Bocco wa Azam aliyefunga mabao 19 ndiye mfungaji bora, refa bora ni Martin Saanya kutoka Morogoro ambaye aliwashinda Oden Mbaga (Dar es Salaam) na Amon Paul (Mara) wakati kocha bora ni Stewart Hall wa Azam aliyewashinda Charles Kilinda (JKT Ruvu) na Charles Mkwasa (Ruvu Shooting). Kila mshindi mepata sh. 3,875,000.
Timu yenye nidhamu bora ni Azam iliyopata sh. 7,750,000, mshindi wa tatu Yanga sh. 15,500,000, makamu bingwa Azam sh. 22,000,000 na bingwa Simba sh. 50,000,000.
Pia Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewazawadia sh. 1,000,000 kila mmoja kwa wachezaji watatu vijana wenye umri chini ya miaka 20 waliofanya vizuri kwenye ligi hiyo.
Wachezaji hao ambao walikuwa kwenye vikosi vya kwanza vya timu zao ni Frank Domayo (JKT Ruvu), Rashid Mandawa (Coastal Union) na Hassan Dilunga (Ruvu Shooting).



Comments