SERIKALI IMEPONGEZA KANISA LA UINJILISTI KWA KUANZISHA CHUO CHA UUGUZI, UKUNGA NA MAABARA MBEYA



SERIKALI imelipongeza Kanisa la Uinjilisti Tanzania lenye makao yake makuu mjini Mbalizi wilaya ya Mbeya mkoani hapa kwa kuanzisha chuo cha uuguzi, ukunga na maabara.

Pongezi hizo zimetolewa leo na Mkuu wa wilaya ya Mbeya Dr. Norman Sigalla wakati wa maafali ya pili ya chuo cha kanisa hilo kilichopo eneo la Ifisi karibu na Hospitali teuele ya wilaya hiyo ambayo nayo inamilikiwa na Kanisa hilo.

Dr. Sigalla alisema kuwa kanisa hilo limekuwa mfano wa kuigwa wa taasisi zingine zisizokuwa za Serikali kwa kutoa taaluma kwa watanzania ambapo katika mahafali hayo wahitimu 117 walitunukiwa vyeti katika fani za uuguzi na maabara.

Aliwasihi wahitimu kutumia vema taaluma zao na viapo huku akisema kuwa wasijiingize katika migomo ya kuwakomoa wagonjwa kutokana na matatizo ya waajiri wao na kwamba migomo inadhihilisha upeo wa mwisho wa kufikiri kwa mwanataaluma na ni kinyume na dini zote zilizopo hapa nchini.

Sanjali na hayo aliziasa taasisi zote za binafsi zinazoanzisha vyuo vya taaluma mbalimbali katika wilaya yake kushirikiana na Serikali za wilaya wakiwemo wakuu wa wilaya ambao ni kiungo na wizara.

Naye Mkuu wa kikosi cha Hospitali ya Jeshi Mbalizi Mbeya Col. Dr. Janga alisema kuwa kuanzishwa kwa chuo hicho na kutoa wahitimu wa fani hizo ni ukombozi kwa taifa kutokana na Taifa kuwa na uhaba wa wataalam wa maabara.

‘’Kwanza kabisa nampongeza sana Mkurugenzi wa Maendeleo wa kanisa hili la Uinjilisti kwa kuanzisha chuo hiki hususani suala la wataalam wa maabara na hata Hospitali hii ya Mbalizi Ifisi ilisaidia sana kuwahudumia wagonjwa wakati wa mgomo wa Madaktari na huu ni mfano wa kuigwa kwa wazalendo’’ alisema Col. Dr, Janga.

Mkurugenzi wa Maendeleo wa kanisa hilo la Uinjilisti Tanzania Mchungaji Marcus Lehner alisema kuwa ataendelea kushirikiana na wapenda maendeleo wote kwa kusaidia hasa vijana kwa kuendeleza vyuo vya ufundi vinavyomilikiwa na kanisa hilo kwa ajili ya kuwaandaa vijana kujiajiri wenyewe pindi wanapohitimu.

‘’Tutaendeleza vyuo vya ufundi maana ni msingi wa ajira kwa vijana na mapungufu yaliyokuwepo kwa upande wa chuo cha uuguzi yote tumejipanga kuyatatua mara moja ikiwemo kuongeza vifaa vya mafunzo ikiwemo darubini, safe cabinete, thermometer, vitabu na walimu wa kudumu’’ alisema Mch. Lehner.

Kwa upande wa wahitimu wa mahafali hayo ya pili, kupitia risala yao iliyosomwa na Shukran Moses na Adolf Mtweve, walisema kuwa wamepata taaluma yao na kuelewa kutokana na chuo hicho kuwa na maabara ya kufanyia mazoezi kwa vitendo, Hospitali ambayo imewasaidia sana na kuwa moja ya darasa lao na kupata elimu ya Kompyuta.


Kwa hisani ya kalulunga

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.