TFF YAOMBOLEZA MSIBA WA MELI Z’BAR

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za ajali ya meli ya Mv Skagit iliyotokea jana (Julai 18 mwaka huu) na kupoteza maisha ya karibu abiria 100 waliokuwemo kwenye chombo hicho.
Ajali hiyo mbaya iliyotokea karibu na Kisiwa cha Chumbe, Zanzibar na kusababisha vifo vya watu wengi ni msiba mkubwa, si kwa wadau wa mpira wa miguu pekee, bali kwa wananchi wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hivyo tunatoa pole na salamu za rambirambi kwa ndugu wa marehemu, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na wote walioathirika na kuguswa na msiba huo mkubwa.
Kutokana na msiba huo, mechi mbili za leo kuwania Klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame) kati ya Atletico ya Burundi na El Salam Wau ya Sudan Kusini na ile ya Mafunzo ya Zanzibar dhidi ya Tusker ya Kenya zitachezwa huku wachezaji wa timu zote wakivaa vitambaa vyeusi.
Mbali ya vitambaa hivyo, pia kutakuwa na dakika moja ya kukaa kimya kwa ajili ya kuomboleza vifo hivyo kabla ya kuanza mechi hizo zitakazochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mechi ya kwanza itaanza saa 8.00 mchana wakati ya pili itachezwa kuanzia saa 10.00 jioni.
 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA