Wanusurika baada ya kukwama baharini

Takriban wakimbizi tisini waliokuwa wamekwama katikati ya bahari ya Mediterranea kwa siku nne, hatimaye wameokolewa, kwa mujibu wa shirika la habari la Italia pamoja na jamaa za wale waliokuwa wamekwama.

Mmoja wa wale waliokuwa kwenye boti hiyo aliwasiliana na idhaa ya kisomali ya BBC kusema kuwa boti yao ilikwama baada ya injini kuisha mafuta na vile vile walikuwa wameishiwa na maji ya kunywa.

Aliongeza kuwa walikuwa wameondoka mji mkuu wa Libya Tripoli, kuelekea pwani ya Italia.

Wahamiaji hao waliokolewa katika mpango wa pamoja kati ya maafisa wa Italia na Libya.

Mapema mwezi huu watu 54 walifariki kutokana na kiu baada ya kuishiwa na maji wakiwa njiani kutoka Libya kuelekea Italia vile vile kwa Boti.

Wahamiaji waliookolewa wamerejeshwa nchini Libya kulingana na taarifa za shirika la habari la Ansa nchini Italia.

Jamaa za wale waliokuwa kwenye boti hiyo walithibitishia BBC kuwa walipatikana.

Wahamiaji wengi kutoka Libya hufariki kila mwaka katika safari zao hatari kuelekea katika kisiwa cha pwani ya Italia cha Lampedusa.
Mmoja wa wahamiaji hao, walisema kuwa walijaribu kuwasiliana na walinzi wa baharini lakini wakapewa nambari nyingine ya simu kupiga ingawa hawakufanikiwa kupata jibu lolote.

Zaidi ya wasomali milioni moja wametoroka nchi yao tangu mwaka 1991, wakati Siad Barre alipompindua rais aliyekuwa mamlakani, na tangu hapo vita havijawahi kuisha nchini Somalia.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*