Kulwa akizungumza katika mkutano huo
Wanahabari wakiwa kazini
Camera woman Faraja Kihongole wa Chanel Tv akiwa kazini
NMB kwa kutambua kuwa watanzania wengi wanaweka akiba ili kutimiza malengo mbalimbali waliyojiwekea yakiwa ni kujenga nyumba,kusomesha watoto na kufikia malengo mengine muhimu maishani mwao, ilizindua promosheni inayowezesha wateja wa NMB Bonus Account an NMB Junior Account kuingia kwenye droo ya kushinda tani ya saruji,mabati ya kuwezeka,amana maradufu,ada za shule,fulana za NMB pamoja na mabegi ya shule kupitia promosheni ya Jenga maisha yako na NMB.
Hivyo basi, leo droo ya Jenga maisha yako na NMB imechezeshwa na washindi zaidi ya 167 wamejishindia zawadi mbalimbali zikiwemo tani za seruji na mabati ya kuwezekea.
Katika picha juu ni Meneja Mawasiliano wa NMB, Josephine Kulwa akifafanua jambo wakati wa kuwatafuta washindi wa droo ya Jenga Maisha Yako na NMB iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Meneja Bidhaa wa Selcom Wireless, Julio Batalia na Mkuguzi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Sadiki Elimsu.
Akizungumza katika hafla hiyo, Meneja Mawasiliani wa NMB,Josephine Kulwa alisema “NMB inaamini promosheni hii sio tu kwamba itaongeza tabia ya kujiwekea akiba lakini pia itasaidia wateja watakaoshinda kufikia malengo waliojiwekea na pia kuboresha maisha yao”
Wateja wote watakaofungua akaunti au kuongeza amana kwenye NMB Bonus Account au NMB Junior Account watapata riba ya kuvutia ambayo inaweza kuwa hadi asilimia 10 kutegemeana na kiwango cha amana zilizowekwa.
Zawadi zilizoshindaniwa kwenye droo ya leo
Zawadi | Namba ya washindi |
Tani ya saruji (simenti) | 8 |
Mabati | 3 |
Double your account | 3 |
Mabegi ya shule | 100 |
Ada zashule | 3 |
Tisheti za NMB | 150 |
Comments