BREAKIING NEWSSSS. MABOMU YA MACHOZI YANAENDELEA KUPIGWA KIGAMBONI BAADA YA WACHIMBA KOKOTO KUFANYA VURUGU NA KUFUNGA BARABARA

HALI sasa si shwari eneo la Mji Mwema, Kigamboni, Dar es Salaam, baada ya wachimba kokoto kufanya vurugu kwa kufunga barabara kwa mawe na kuwasha matairi barabaran wakipinga kitendo cha Serikali kuwazuia kuchimba kokoto.

Mkazi mmoja wa Mji Mwema aliye karibu na makazi ya Rais msitaafu wa wa Zanzibar Alhaji Aboud Jumbe, amesema hali ni mbaya kiasi cha asilimia kubwa ya wakazi wa eneo hilo kujifungia majumbani wakihofia vurugu hizo.

"Ndugu mwandishi wa habari, hali hivi sasa ni mbaya mno, mawasiliano ya usafiri yamekatika kwani wachimba kokoto waliozuiwa kufanya kazi yao, wameandamana huku wengine wakijaza kokoto na mawe barabarani na wengine wakichoma matairi, tunaogopa hivyo tumejifungia majumbani" alisema mama huyo.

Alisema mabomu ya machozi yanaendelea kupigwa na FFU ili kuwatawanya vijana hao, lakini inaelekea ni wabishi.

Blogu yako ya Kamanda wa Matukio itaendelea kuwapatia taarifa juu ya sakata hilo kwa kadri itakavyokuwa inazipata.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*