Mastaa wetu wa filamu hapa nchini, wametokelezeaje sasaaa
 Wema Sepetu akijiweka sawa.
Wema Sepetu pia akizungumzia ujio wao ndani ya mji wa Moshi, kuwa wao kama Wasanii Nyota wa Filamu wamewasili mkoani humo kusaka vipaji vipya mbalimbali vya filamu, usahili huo unafanyika kwenye ukumbi wa Mr Price, ulioko mtaa wa Malindi.
Mmoja wa wasanii mahiri katika fani ya uigizaji hapa nchini, Wema Sepetu akifanya mahojiano mafupi na Millard Ayo wa Clouds FM mapema leo kwenye amsha amsha ya tamasha la Serengeti Fiesta ambalo linafanyika jioni ya leo mpaka lyamba ndani ya uwanja wa chuo cha Ushirika,ndani ya mji wa Moshi, ambapo katika tamasha hilo kiingilio kimepangwa kuwa ni nusu mnyama tu a.k.a 5,000/= kwa kila kichwa.
Msanii mwingine nyota katika tasnia ya filamu, Aunt Ezekiel akielezea ni namna tamasha la Serengeti Fiesta lilivyowambamba wakazi wa mji wa Moshi na vitongoji vyake, na pia ujio wao kuwatafuta wasanii wapya chipukizi katika tasnia hiyo ambayo imekuwa ikikua siku hadi siku.
Millard Ayo akifanya mahojiano na Ray a.k.a Vincent Kigosi kuhusiana na ujio wao ndani ya mji wa Moshi
Jacob Steven a.k.a Steven akifafanua jambo mapema leo mtaa wa Malindi kuhusiana na suala zima la wasanii hao kulivamia jiji la Moshi.
Wema na Steve Nyerere Wakiwa katika mazungumzo yao ya hapa na pale.
  Kiongozi wa msafara wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012, Mully B akiwa na mastaa wa filamu, Wema Sepetu na Aunt Ezekiel afu fulllll BBM kama kawa.
 Wema Sepetu katika pozi na washabiki wake mapema mchana huu.
 Pichani ni Gari aina ya Vits itakayotolewa jioni ya leo kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012, kwa mshindi atakaejishindia kwenye droo itakayofanyika katika uwanja wa chuo cha ushirika, ambako tamasha hilo litarindima mpaka majogoo.
Mtangazaji wa Clouds FM,Millard Ayo akiwa Live mapema leo mtaa wa Malindi katika mpango mzima wa amsha amsha kwa wakazi wa Moshi kuhusiana na tamasha la Serengeti Fiesta 2012, ambapo pia katika tamasha hilo kutatolewa zawadi mbalimbali ikiwemo gari ndogo aina ya Vits kama uinavyo pichani ikinadiwa vilivyo. 
Kawa kawa amsha amsha ya tamasha la Serengeti Fiesta pia linatoa mafuta kwa magari daladala,pikipiki sambamba na baji lita 10 ama tano kutoka kampuni ya GAPCO ambao pia ni sehemu ya wadhamini wa tamasha hilo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI