GARI MOSHI LAWAKA MOTO INCHINI INDIA HUKU WATU ZAIDI YA 30 WAKIUAWA

Treni ikiteketea kwa moto wakati juhudu za uokozi zikiendelea

 WATU zaidi ya 30 wameuawa Kusini mwa India katika mji wa Chennai kwa kuteketea kwa moto baada ya gari moshi walilokuwa wanasafiria kuwaka moto Julai 30, 2012. 

Mkasa huo umetokea Jumatatu asubuhi wakati gari moshi hilo lilipokuwa linatokea mjini New Delhi na kusababisha abiria wengine zaidi ya 20 kujeruhiwa na kukimbizwa hospitalini.

Maafisa wa uokoaji kwa sasa wanaendelea na shughuli za kuwatafuta watu zaidi ambao huenda wamekwama ndani ya gari moshi hilo huku idadi ya wafu ikitarajiwa kuongezeka.

Walioshuhudia mkasa huo wanasema, waliona gari moshi hilo likiwaka moto likiwa safarini, mkasa ambao umeleta kumbukumbuku ya ajali nyingine ya gari moshi iliyotokea mwezi Mei mwaka huu baada ya magari Moshi kugongana na kusababisha zaidi ya watu 20 kuuawa.

Taasisi inayoshughulika na maswala ya ajali za terni nchini humo inasema kuwa tangu mwaka 2009,  watu 25,705 wameuawa kutokana na ajali za gari moshi.

Ajali mbaya zaidi ya gari moshi iliyowahi kuikumba nchi hiyo ilikuwa mwaka 1981 ambapo watu 800 waliuawa baada ya gari moshi la abiria kuzama katika mto katika jimbo la Bihar.

Serikali ya India inasema iko katika harakati za kuimarisha sekta ya safari za reli kwa kuimarisha usalama wa magari moshi.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA