JK AWAAPISHA WATENDAJI WAKUU WA MAHAKAMA

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo amemwapisha Mtendaji mkuu wa Mahakama pamoja na Msajili mkuu wa Mahakama na msajili wa mahakama ya rufani katika hafla fupi iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam.Walioapishwa leo ni Mtendaji mkuu wa Mahakama Bwana Hussein Katanga,Msajili Mkuu wa Mahakama Bwana Ignus Paul Kitusi na Msajili wa Mahakama ya Rufani Bwana Panterine Muliisa Kente.Pichani Mtendaji mkuu wa Mahakama Bwana Hussein Katanga akila kiapo mbele ya Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue(kushoto) pamoja na maofa waandamizi wa mahakama aliowaapisha leo asubuhi ikulu jijini Dar es Salaam.(Wapili kushoto) ni Mtendaji mkuu wa Mahakama  Bwana Hussein Katanga,(Wanne kushoto) ni Msajili Mkuu wa Mahakama Bwana Ignus Paul Kitusi na kulia ni Msajili wa Mahakama ya Rufani Bwana Panterine Muliisa Kente(picha na Freddy Maro)

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*