KIKOSI CHA YANGA CHAENDA RWANDA KWA MWALIKO WA KAGAME

Kikosi cha Yanga.
Kikosi kizima cha timu ya Yanga ya jijiji Dar es Salaam, kimeondoka leo jijini kuelekea nchini Rwanda ambako kitaweka kambi kwa ajili ya mazoezi yake ya kujiandaa na Ligi Kuu ya Tanzania Bara, inayotarajia kuanza mwezi ujao. 

Mbali kambi hiyo pia kikosi hicho kimepata mwaliko wa Rais wa Rwanda Paul Kagame, ambapo kikosi hicho kikiogatngozana na viongozi wake kitatinga Ikulu ya nchini humo kwa ajili ya kutambulisha Kombe lao la ushindi wa michuano ya Kombe la Kagame, iliyomalizika mwezi uliopita. 

Kikiwa nchini humo kikosi hicho kinatarajia kucheza michezo mitatu ya kirafiki ambapo mchezo wa kwanza utakuwa ni kati yao na timu ya Royal Sports, mchezo wa pili utakuwa na Polisi na wa tatu utapangwa baada y mchezo wao wa kwanza.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI