''Marekani haikuhusika na mauaji ya mhubiri''


Vurugu Mombasa

Ubalozi wa Marekani mjini Nairobi umekanusha madai ya kuhusika na mauaji ya kiongozi mmoja wa kidini mjini Mombasa, Sheikh Aboud Rogo.

Wakili wa Rogo, Mbugua Mureithi na viongozi wengine wa Kiislamu wamedai kuwa Marekani ilihusika na mauaji ya kiongozi huyo wa kidini aliyepigwa risasi na watu wasiojulikana mjini Mombasa.

Makanisa kadhaa yaliteketezwa na makundi ya vijana waliokuwa wakipinga mauaji hayo.
Lakini ubalozi huo umesema madai hayo hayana msingi wowote.

Hali imetulia mjini Mombasa baada ya usiku wa makabiliano mapya mjini humo kufuatia shambulizi la guruneti ambapo mtu mmoja aliuawa na wengine wengi kujeruhiwa.

Shambulio hilo limefuatia muda wa utulivu baada ya siku mbili ya makabiliano makali kati ya vijana waliofanya maandamano na polisi ambapo maafisa wanne wa polisi waliuawa.

Ghasia hizo zilisababishwa na kuuawa kwa mhubiri wa kiislamu Aboud Rogo Mohammed,aliyetuhumiwa na umoja wa mataifa pamoja na Marekani kuwa na uhusiano na makundi ya kigaidi

Mkuu wa polisi katika mkoa wa pwani ni Aggrey Adoli ameithibitishia BBC tukio hilo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI