''Marekani haikuhusika na mauaji ya mhubiri''
Ubalozi wa Marekani mjini Nairobi umekanusha madai ya kuhusika na mauaji ya kiongozi mmoja wa kidini mjini Mombasa, Sheikh Aboud Rogo.
Makanisa kadhaa yaliteketezwa na makundi ya vijana waliokuwa wakipinga mauaji hayo.
Lakini ubalozi huo umesema madai hayo hayana msingi wowote.
Hali imetulia mjini Mombasa baada ya usiku wa makabiliano mapya mjini humo kufuatia shambulizi la guruneti ambapo mtu mmoja aliuawa na wengine wengi kujeruhiwa.
Shambulio hilo limefuatia muda wa utulivu baada ya siku mbili ya makabiliano makali kati ya vijana waliofanya maandamano na polisi ambapo maafisa wanne wa polisi waliuawa.
Ghasia hizo zilisababishwa na kuuawa kwa mhubiri wa kiislamu Aboud Rogo Mohammed,aliyetuhumiwa na umoja wa mataifa pamoja na Marekani kuwa na uhusiano na makundi ya kigaidi
Mkuu wa polisi katika mkoa wa pwani ni Aggrey Adoli ameithibitishia BBC tukio hilo.
Comments