MATOKEO MABOVU OLMPIKI 2012 YAMKERA RAIS NIGERIA


LAGOS, Nigeria
 KUFUATIA Nigeria kuvurunda na kurudi bila hata medali moja ya mashindano ya Olimpiki 2012 jijini London, rais wa nchi hiyo Goodluck Jonathan ameagiza mageuzi na  mabadiliko makubwa na ya haraka katika tasnia ya michezo, kupitia wizara husika.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Habari wa Nigeria, Labaran Maku, wakati wa mkutano wake na vyombo vya habari uliofanyika Ikulu ya nchi hiyo, baada ya kikao cha kila wiki cha Rais na Baraza Kuu la Utendaji (FEC) Jumatano.
Waziri Maku alisisitiza kuwa, rais amesikitishwa kwa kilichofanywa na wawakilishi wa nchi hiyo jijini London, na kwamba ametaka kuwapo kwa haja ya kubadili mwenendo huo mbovu.
Kwa mujibu wa waziri Maku, rais Jonathan, ameagiza kuwapo kwa utaratibu wa wizara na vyama vya michezo kushirikisha serikali za majimbo, sekta binafsi na wadau wengine, ili kuweka kipaumbele cha mafanikio ya michezo nchini humo.
"Yeye (rais Jonathan) amesema kufanya kwetui vibaya jijini London, kuchukuliwe kama changamoto ya ya harakati mpya za kuirejeshea heshima michezo ya nchi hiyo ambayo, imeanza kupotea kutokana na lindi la kuvurundano kwenye mashindano makubwa.
"Rais Jonathan anaamini kwamba ili kubadili mazingira na hali ya sasa ya kufanya vibaya, tunahitaji wataalamu, tunahitaji mipango yakinifu na tunahitaji kufadhili michezo katika mfumo utakaowezesha nchi kurejesha mvuto na maendeleo katika sekta hiyo.
"Yeye anaamini kwamba katika mashindano yajayo ya Jumuiya ya Madola na Olimpiki ijayo ya mwaka 2016 nchini Brazil, lazima Nigeria kama taifa lilenge kutimiza malengo binafsi kayika ukuzaji wa michezo ili kuimarisha ushiriki wa wawakalishi," alisisitiza Waziri Maku.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU