MECHI ZA MICHUANO YA BancABC SUP8R KUENDELEA KESHO

Mechi za michuano ya BancABC SUP8R inayoshirikisha timu nane bora kutoka Tanzania Bara na Zanzibar zinaendelea kesho (Agosti9 mwaka huu) kwenye miji ya Dar es Salaam, Moshi, Mwanza na Zanzibar.

  Mkurugenzi wa Mashindano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Saad Kawemba na viongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA) chini ya Rais wao Amani Makungu walikutana leo mjini Zanzibar kuzungumzia maendeleo ya michuano hiyo. Viongozi wengine wa ZFA waliohudhuria kikao hicho ni Katibu Mkuu Kassim Haji Salum na wajumbe saba wa Kamati ya Utendaji.

  Katika kundi A Jamhuri itacheza na Zimamoto kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar kuanzia saa 2 kamili usiku, wakati Simba itaparurana na Mtende kwenye Uwanja wa Ushirika, mjini Moshi. Mechi hiyo itaanza saa 10 kamili jioni.

  Azam itakuwa mwenyeji wa Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam wakati Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza utakuwa mwenyeji wa mechi ya Polisi Morogoro na Super Falcon. Mechi hizo zote za kundi B zitaanza saa 10 kamili jioni.

  Hatua hiyo ya makundi itamalizika Agosti 12 mwaka huu kwa mechi nne. Simba na Zimamoto zitaoneshana kazi Uwanja wa CCM Kirumba wakati Jamhuri na Mtende zitacheza kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.

  Mechi za kundi B zitakuwa kati ya Super Falcon na Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Amaan na Azam dhidi ya Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Ushirika.

  Boniface Wambura

Ofisa Habari

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI