MSAMA AMSAIDIA SH. MILIONI MOJA MCHEZAJI WA ZAMANI WA SIMBA,TAIFA STARS, ALPHONCE MODEST KWA AJILI YA MATIBABU YA MIGUU

 Mratibu wa Tamasha la Injili la Pasaka Tanzania, Alex Msama (kushoto), akimkabidhi msaada wa sh. mil. 1, mchezaji wa zamani wa Simba na Taifa Stars, Alphonce Modest za kusaidia matibabu ya miguu inayosumbuliwa na baridi yabisi. Msaada huo uliokabidhiwa Dar es Salaam leo, ulihamasishwa na Mhariri Kiongozi wa gazeti la Champion, Saleh Ali (wa pili kushoto) pamoja na Mtangazaji wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten na Radio Magic FM, Said Kilumanga (wa pili kulia). Wameiomba Jamii yenye huruma kumsaidia kwa hali na mali mchezaji huyo ambaye wamemsafirisha kwa gharama zao kutoka Mwanza. (PICHA ZOTE NA KAMANDA  RICHARD MWAIKENDA)
Modest akitembea kwa taabu huku akisaidiwa na mdogo wake Francis

Jinsi alivyo kwa sasa Modest
 Alex Msama akielezea jinsi alivyoguswa kumsaidia Modest na kutoa mwito kwa watanzania kumuunga mkono kwa kumsaidia mchezaji huyo wa zamani ambaye anahitaji fedha za kumtibia katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI)
Modest akitoa shukrani kwa Msama na kuelezea jinsi ugonjwa huo ulivyompata na kumsababishia kulazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Mwanza kwa mwaka mzima wa 2011
 Kilumanga ambaye ni mmoja wa wahamasishaji  waliowezesha kupatikana msaada huo kutoka kwa Msama, akiendelea kuuhamasisha umma kmsaidia kwa hali na mali Modest apate kupona.
Saleh Ali ambaye pia ni mmoja wa wahamasishaji, akiwaomba wasamaria wema kuendelea kumsaidia Modesti kwa hali na mali.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI