Mwanahabari na Mhariri wa siku nyingi, Alfred Mbogora amefariki Dunia leo

Habari zilizotufikia kutoka Baraza la Habari Tanzania (MCT) kwamba mmoja wa maofisa wake na Mwanahabari na Mhariri wa siku nyingi, Alfred Mbogora (pichani), amefariki Dunia leo saa 11.00 alfajiri katika hosipitali ya Taifa ya Muhimbili.

Katibu Mtendaji wa MCT, Kajumbi Mukajanga amesema kwamba Mbogora alilazwa Muhimbili tangu Jumanne baada ya kuwa ameanguka katika eneo la Tegeta, mara baada ya kupata chakula wakiwa njiani kwenda Bagamoyo kwa shughuli za kikazi.

Kabla ya kuanguka, Mbogora alikuwa akilalamika kwamba anasikia kuishiwa nguvu kwenye mguu na mkono na alipojaribu kusimama ili kutembea kutokana na hali aliyokuwa akiisikia mwilini alianguka.

Tangu wakati huo (baada ya kuanguka) alikata kauli na hakuwa kusema chochote hadi hapo alipokata roho leo alfajiri. Ni pigo kwa sekta ya habari nchini, kumpoteza mwanahabari mwenzetu ambaye ametoa mchango mkubwa katika sekta yetu ya habari.

Inasadikiwa kwamba msiba wa Mbogora uko nyumbani kwake Segerea, lakini taarifa zaidi tutazipata kadri tutakavyoendelea kuwasiliana na MCT pamoja na familia ya marehemu.

Tunachukua fursa hii kuwapa pole wafiwa wote, kwanza ni familia ya marehemu, MCT na wanahabari wote nchini. Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake luhimidiwe, Amen.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU