Tanzania itafuta usajili wa meli za Iran

Serikali ya Tanzania inasema meli za mafuta 36 za Iran zimesajiliwa tena nchini Tanzania, ili kujaribu kuhepa vikwazo dhidi ya Iran vilivowekwa na Marekani na Umoja wa Ulaya.
Uchunguzi uliofaywa na serikali ya Tanzania, ambao ulionekana na shirika la habari la Reuters, unaonesha kuwa serikali haikujua lolote kuhusu shughuli hizo za kuzipatia meli za mafuta za Iran bendera ya Tanzania - shughuli iliyokuwa ikifanywa na wakala alioko Dubai.

Mafuta ya Iran yamewekewa vikwazo, ili kuishawishi Iran iache mradi wake wa nuklia.
Tanzania imeacha kuagiza mafuta kutoka Iran.
Uchunguzi ulifanywa na serikali ya Tanzania, baada ya mbunge mmoja wa Marekani, Howard Berman, mwenyekiti wa kamati ya Congress ya maswala ya nchi za nje, kueleza wasiwasi wake juu ya meli hizo za Iran kupatiwa bendera ya Tanzania.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*