Walimbwende 15 wa Miss Ilala 2012 kutambulishwa Club ya Nyumbani Lounge kesho

Mkurugenzi wa Machozi Entertainment, Gadner G. Habash
KAMATI ya maandalizi ya shindano la Miss Ilala 2012, kesho Alhamis saa 5 asubuhi, itatambulisha mbele ya wanahabari warembo 15, wanaowania umalkia wa taji hilo, linaloshikiliwa na Vodacom Miss Tanzania, Salha Israel.

Warembo hao kutoka vitongoji vya Dar City Center, Tabata na Ukonga wamekuwa katika kambi hiyo kwa wiki mbili sasa na wamekuwa wakiendelea na mazoezi katika Club ya Nyumbani Lounge, iliyopo maeneo ya Namanga, Dar es Salaam sehemu ambayo kesho itatumika katika hafla hiyo fupi ya utambulisho.

Miss Ilala 2008, Slyvia Mashuda ndiye mkufunzi wa warembo hao na ikumbukwe Slyvia alishika nafasi ya pili katika Miss Tanzania mwaka ambao Nasreen Karim alitwaa taji la Miss Tanzania.

Wadhamini waliothibitisha katika mashindano hayo ni pamoja na City Sports Lounge, gazeti la Jambo Leo, Nyumbani Lounge, 100.5 Times FM, Uhuru One na 88.4 Cloud's FM na Redds Premmium Cold. Miss Ilala 2012 Itafanyika Septemba 7, mwaka huu katika sehemu ya nje ya Nyumbani Lounge.

Imetolewa na:
Gadna G. Habash
Mkurugenzi Machozi Entertainment

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA