WATANZANIA WAISHIO LONDON NCHINI UINGEREZA KUJUMUHIKA NA WENZAO WA AFRIKA YA MASHARIKI KATIKA HAFLA FUPI YA UFUNGUZI RASMI WA SHUGHULI ZA BENKI YA KCB HAPA NCHINI UINGEREZA

 Mheshimiwa Balozi, akiwa kwenye picha ya pamoja na Wawakilishi wa Benki ya KCB Tanzania LTD. Pili (Kulia), Balozi Peter Kallaghe, (kwanza kulia) Dada Shose Kombe, Bwana James Agin, Dada Pamela Baguma na Naibu Balozi, Mh. Chabaka Kilumanga
Wawakilishi kutoka Benki ya Biashara ya Kenya (KCB) wakijiorodhesha kwenye Kitabu cha Wageni, walipo karibishwa kwenye Ofisi za Ubalozi wa Tanzania na Mheshimiwa, Balozi, Peter Kallaghe na Naibu wake , Mheshimiwa, Chabaka Kilumanga, kwa mazungumzo mafupi. Mhe. Balozi, alitaka kufahamu madhumuni ya safari ya wawakilishi hao wa KCB hapa nchini Uingereza, na kutaka kukutana na Wananchi wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki. 

Benki hiyo kubwa Afrika Mashariki, imepata mafanikio na maendeleo makubwa yaliyopatikana kwa kutumia Teknolojia ya Kisasa ya kuweza kutuma na kupokea Pesa kwa njia ya mtandao (Internet), Simu za mkononi na nyinginezo kwa ghalama nafuu zaidi, kulinganisha na njia nyingine za utumaji na kupokea fedha.
-
UBALOZI WA TANZANIA, LONDON, KWA NIABA YA BENKI YA BIASHARA KENYA (KENYA COMMERCIAL BANK (KCB)) INAWAALIKA WATANZANIA WOTE WAISHIO UINGEREZA, KUJA KUJUMUHIKA NA WENZAO WA AFRIKA YA MASHARIKI KATIKA HAFLA FUPI YA UFUNGUZI RASMI WA SHUGHULI ZA BENKI YA KCB HAPA NCHINI UINGEREZA, KWA WAISHIO UGHAIBUNI (DIASPORA). 

HAFLA HIYO FUPI YA UFUNGUZI AMBAYO ITAWAJUMUISHA  WAAFRIKA MASHARIKI, INA LENGO LA KUPANUA WIGO WA SHUGHULI ZA BENKI YA KCB HAPA UINGEREZA, KUTANGAZA SHUGHULI ZA UTENDAJI WAKE KATIKA KUWASAIDIA WANANCHI WA JUMUHIYA YA AFRIKA YA MASHARIKI KATIKA KUWEKEZA KIBENKI, KUFUNGUA AKAUNTI ZA AINA TOFAUTI, KUJIWEKEA AKIBA, NJIA MBALIMBALI ZA KUTUMA NA KUPOTEKEA PESA KWA NJIA YA MTANDAO (INTERNET), KUTUMA PESA KWA KUTUMIA SIMU ZA MKONONI (MOBILE PHONES), IPADS NA NYINGINEZO. 

HALFA HIYO FUPI, ITAFANYIKA SIKU YA JUMAMOSI 4 AUGUST 2012, KUANZIA SAA 16:00pm, KWENYE HOTEL YA HOLIDAY INN, BLOOMSBURY, CORAM STREET, LONDON, WC1N 1HT

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.