ZUMA ATANGAZA MAOMBOLEZO YA WACHIMBA MIGODI WALIOUAWA NA POLISI

Baadhi ya miili ya wachimba migodi waliuawa na askari Afrika Kusini

 Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma ametangaza kipindi cha maombolezo nchini humo kufuatia mauaji ya wachimba madini thelathini na wanne yaliyofanywa na polisi,

wakati walipokuwa wakiandamana kudai malipo bora zaidi ya kazi.
Bwana Zuma pia ametaka tume ya uchunguzi ya kisheria ichunguze mauaji hayo katika mgodi wa madini meupe yaani PLATINUM eneo la Marikana.

Wakati huohuo wachimba madini wameamriwa kurejea kazini siku ya Jumatatu la sivyo watafukuzwa kazi.

Lakini wengi wamesema kumaliza mgomo wao sasa ni sawa na kuwadhalilisha wenzao waliouawa.

Wanasema watarejea kugoma katika eneo la mgodi huo na wataendelea kushinikiza malipo bora zaidi ya kazi.

Hata hivyo chama cha wafanyakazi wa migodi cha NUM ambacho kina uhusiano wa karibu na chama tawala cha ANC - kinasema wanachama wake wamekubali kurejea kazini.

Mmoja wa wachimba madini hao Vuyisile Mchiza, amesema atarejea kazini iwapo idadi kubwa ya wenzake watakubaliana kusitisha mgomo.

''Iwapo idadi kubwa watarejea kazini kesho, basi na mimi nitakwenda''. Anasema. ''Iwapo wengi hawatakwenda kazini, nami pia sitakwenda, kwasababu sitaweza kufanya kazi wakati wengine wakiwa bado wanaomboleza''. Ameongeza.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.