BAADA YA NCHI JIRANI MWANAMKE KUZAA NA BABA YAKE WATOTO WATATU, SASA HUKU MBEYA BABA MZAZI (39) AMPA MIMBA MWANAE WA KUMZAA MWENYE UMRI WA MIAKA 15
Habari na
Ezekiel Kamanga,Mbeya.
Mkazi wa
Mtaa wa Mbete,Kata ya Isanga Jijini Mbeya Bwana Yussuf Hamad(39),anatuhumiwa
kumpa mimba binti yake wa kumzaa(15) jina lake limehifadhiwa.
Hayo
yamethibitishwa na Mama mzazi wa binti huyo Bi, Regina Simon(35) baada ya kupata
taarifa Mei 11 mwaka huu kuwa binti yake ana ujauzito wa miezi minne,na kuamua
kutoa taarifa kwa Balozi wa mtaa huo Bwana Steven Ovaova ambaye naye alitoa
taarifa kwa Mwenyekiti wa Kitongoji Bwana Angelo Sanga.
Viongozi
hao wa mtaa walimuita mtuhumiwa na ili kupata ukweli wa tukio hilo,lakini
mtuhumiwa alikanusha ingawa binti yake alithibitisha kutendewa ukatili huo na
kwamba alikuwa akitishiwa kwa mapanga kila alipokuwa akifanya naye tendo la
ndoa.
Baada ya
uongozi kupata maelezo kutoka kwa binti huyo na mzazi kukataa waliamua kuipeleka
kesi hiyo Polisi,ambapo walitoa PF3 iliyomwezesha binti huyo kupelekwa kwa
daktari ambaye alithibitisha kuwa binti huyo ana ujauzito.
Hata
hivyo hivi sasa binti huyo amelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mbeya akisubiri
kujifungua ingawa umri mdogo wa binti huyo amekuwa chini ya uangalizi wa karibu
wa daktari hospitalini hapo.
Mtuhumiwa
atafikishwa mahakamani Septemba 25 mwaka huu katika mahakama kuu jijini hapa,ili
kujibu tuhuma zinazomkabili kesi inayotarajiwa kusikilizwa na hakimu wa mahakama
hiyo mheshimiwa Majige.
Comments