DROGBA; BADO 'NIPO NIPO' SHANGHAI SHENHUA

SHANGHAI, Shenhua
“Nimeikumbuka sana Ligi Kuu ya England, kwa sababu ni moja ya ligi kubwa na bora duniani, lakini ukweli ni kwamba, sijutii uamuzi wangu wa kuja hapa Shanghai”
MSHAMBULIAJI Didier Drogba kwa mara ya kwanza amekanusha tetesi zinazomuhusisha na uwezekano wa kurudi kukipiga katika moja ya klabu za Ligi Kuu za England.
Nyota huyo wa kimataifa wa Ivory Coast, aliihama klabu bingwa barani Ulaya Chelsea, na kutua Shanghai Shenhua ya hapa China katika usajili uliopita wa majira ya joto barani Ulaya.
Ukata na tatizo la kipesa lililotajwa kuikumba klabu ya Shanghai inayoshiriki Ligi Kuu ya China, ukadaiwa kuziweka vitani klabu mbioli za Arsenal na Liverpool katika jaribio la kupata saini ya Drogba – na sasa kauli hii inaziweka mbali klabu hizo.
Lakini mkali huyo aliyefunga fainali na kuipa Chelsea ubingwa wa Ulaya kabla ya kutimka ameibuka na kusisitiza kuwa anayapenda kwa ujumla maisha ya ndani na nje ya uwanja akiwa na klabu yake mpya.
“Niseme kweli nina furaha kuwa hapa, hivyo sina hata sababu ya kuondoka. Sitaki kabisa kuihama klabu hii.
“Nataka kuendelea kubaki hapa muda mrefu kadri nitakavyoweza, kushinda baadhi ya mataji nikiwa na timu yangu na kuwafanya mashabiki wafurahie uwapo wangu.
“Najua ni ngumu kutimiza ndoto hizo kwa sasa, lakini najua kwamba kuna tumaini hilo na naamini pia kuwa nitaendelea kuwa sehemu ya kikosi kumalizia mkataba wangu na Shanghai.
Akaongeza kuwa: “Mkataba wangu hapa ni wa miaka miwili na nusu, labda na zaidi. Labda na zaidi na natumaini itakuwa zaidi kwa sababu nina furaha ya kweli hapa.
“Nimeikumbuka sana Ligi Kuu ya England, kwa sababu ni moja ya ligi kubwa na bora duniani, lakini ukweli ni kwamba, sijutii uamuzi wangu wa kuja hapa,” akamaliza Drogba aliyeshinda tuzo ya Tallent O’dor hivi karibuni

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI