Mshindi wa Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Bububu Husein Ibrahim Makungu
(BHAA) akionesha cheti chake cha ushindi baada ya kutangazwa na Tume ya
Uchaguzi ya Zanzibar kuwa mshindi wa Uchaguzi huo.
Mshindi wa Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Bububu Husein Ibrah Makungu(BHAA)
akitoa shukrani kwa ushindi wake na kuwapongeza wapiga kura wake kwa
kumpa ushindi ili kuliongoza jimbo hilo kwa maendeleo ya Wananchi wa
Jimbo hilo.
Msimamizi wa Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Bububu akimkabidhi Cheti
mshindi wa uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi Hussein Ibrah Makungu, baada
ya kutangaza matokeo ya uchaguzi huo katika Ukumbi wa Chuo Kikuu cha
Taifa SUZA Betras.
mwonekano wa matokeo
Maofisa wa Uchaguzi Mdogo Jimbo la Bububu wakijumuisha kura katika
kituo cha kujumlishia kura zote kilichokuwa katika Chuo cha Taifa SUZA
Betras.
Msimamizi wa Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Bububu akitoa matokea ya Uchaguzi katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa SUZA,Betrais Betrais
Mgombea wa Chama cha Mapinduzi Hussein Ibrahim Makungu na Viongozi
wengine wa Vyama vilivyoshiriki Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Bububu
wakifuatilia matokeo ya Uchaguzi.
Viongozi wa Vyma vya Siasa wakifuatilia Matokeo ya Uchaguzi.
Wasimamizi wa Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Bububu kutoka Nje wakifuatilia
Ujumlishaji wa Kura katika chumba cha kujumlishia Kura Betras.
Kiongozi wa Chama cha Wakulima Mchenga, akitowa shukrani kwa nia ya Mgombea wake hakufika katika chumba cha kutolea matokeo.
Aliyekuwa Mgombea wa Uchaguzi jimbo la Bububu kwa tiketi ya Chama cha
CUF, Issa Khamis Issa, akitowa malalamiko yake kutokana na kushindwa
kwake na Mgombea wa CCM,Hussein Ibrahim Makungu(BHAA) baada ya
kutangazwa mshindi wa Uchaguzi huo. katika ukumbi wa Chuo cha Taifa cha
SUZA Betras.
Mgombea wa Chama cha ADC Zuhura Bakari Mohammed, akitowa shukrani kwa
wananchi waliompigia kura katika uchaguzi huo, baada ya kutolewa matokea
ya uchaguzi wa Bububu. Chanzo; Haki Ngowi Blog
Comments