Katibu
wa NEC,Itikadi na Uenezi Taifa wa CCM,Nape Nnauye,alipokuwa akizungumza
na Waandishi wa habari jana kuhusu Kufanyika kwa Vikao vya juu vya
Chama hicho katika Ukumbi wa White House mjini Dodoma,vikijadili majina
ya wagombea nafasi mbali mbali zikiwemo,Uwenyekiti wa Wilaya na Mikoa
na Ujumbe wa Halamashauri Kuu ya Taifa.
Nape
Nnauye akiwalekeza jambo waandishi wa habari wakati alipokuwa akiongea
nao mjini Dodoma jana.Picha na Ramadhan othman-Dodoma
--
Na Rajab Mkasaba,
Na Rajab Mkasaba,
Dodoma
VIKAO
vya ngazi ya juu vya Chama Cha Mapinduzi (CCM), chini ya Mwenyekiti
wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete
vinandelea hapa mjini Dodoma vikiwa na ajenda kuu ya uchaguzi ndani ya
chama hicho.
Viongozi
mbali mbali wa chama hicho wapo mjini hapa kwa lengo la kushiriki vikao
hivyo akiwemo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.
Dk. Ali Mohamed Shein.
Miongoni
mwa shughuli kubwa za vikao hivyo ni pamoja na kuchuja majina ya
wagombea walioomba kuteuliwa na chama hicho katika nafasi kadhaa
zikiwemo nafasi za Uwenyekiti wa Wilaya, Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya
Taifa ngazi ya Wilaya na Uwenyekiti wa Mkoa.
Kamati
Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM,inatarajiwa kuanza kikao chake
kuanzia kesho na keleza kuwa kutokana na mabadiliko ndani ya chama
hicho hivi sasa Wajumbe wa NEC pia,watatoka katika Wilaya.
Alieleza
kuwa nafasi nyengine ni za Wenyeviti wa Mikoa, Katibu wa uchumi na fedha
wa Mkoa, nafasi za U-NEC kitaifa, ambazo 10 I kutoka Bara na 10 kutoka
Zanibar.
Kwa upande
wa Zanzibar Katibu huyo, alisema kuwa pia kuna Wajumbe wa NE wanaotoka
Wilayani na Mikoani na kusisitiza kuwa tayari majina ya wagombea mbali
mbali kutoka Jumuiya za Chama za UVCCM, Wazazi na UWT yameshapitiwa na
hivi sasa yameshaanaliwa kwa ajili ya kusubiri vikao vya uwamuzi.
Wakati huo
huo, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye amesisitiza kauli
yake ya kuwa yeye yuko tayari kutoa taarifa wakati wowote zinapotakiwa
taarifa hizo na waandishi.
Alieleza
kusikitishwa na tabia ya baadhi ya vyombo vya habari vinavyotoa taarifa
kutoka kwa watu wa pembeni ambao sio wasemaji wa chama hicho ambapo
hatimae husababishwa kutolewa taarifa zenye utata na zenye kujikia
upande mmoja.
Nape
aliyasema hayo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari leo
mjini Dodoma na kueleza kuwa ni vizuri kukaandikwa habari za uhakika na
kuachana na zile habari za watu wa pembeni ambazo aghalabu huwa I habari
za kutumiwa na watu.
Katika
maelezo yake, Nape alieleza kusikitishwa na tabia hiyo ya baadhi ya
vyombo vya habari na kusisitiza kuwa yeye masaa yote 24 yuko tayari kutoa taarifa hata saa tisa za usiku.
“Mimi niko tayari kutoa taarifa wakati
wowote na iwapo ukiandika habari ya kupewa na mtu ujue kuwa hali hiyo
ndio inayosababisha makundi kwani ni taarifa za mlengo mmoja, na ukipewa
nitafuate ili nikuthibitishie na hatimae upate kuandika kitu chenye
uhakika wa pande zote mbili”,alisema Nape.
Nape
alisema kuwa kutokana na azma ya kuwarahisishia waandishi wa habari kuwa
wanapata taarifa sahihi na kuzirusha kwa wakati afisi yake inampango wa
kuweka karibu huduma zote za kutuma habari yakiwemo mawasiliano ya mtandao.
Alisema
kuwa yeye akiwa pamoja na maafisa wa kitengo chake wamekusudia kuchukua
hatua hiyo kwa kutambua kuwa afisi yake ina dhima ya kutunza taswira ya
Chama Chama Mapinduzi (CCM), hivyo kuandika habari zisizosahihi
hazitokipendezesha chama chake.
Comments