KUELEKEA PAMBANO LA WATANI; MARA NYINGI YANGA HUFUNGWA USIKU
Na Mahmoud Zubeiry
MECHI ya Jumatano ya watani wa jadi, Simba na Yanga itaanza saa 11:00 jioni na itamalizika kuanzia saa 1:00, wakati giza limekwishaingia uwanjani. Je, unajua matokeo ya mechi zilizopita za watani zilizoishia gizani? BIN ZUBEIRY yupo kwa ajili yako, pata vituz.
MATOKEO YA MECHI ZA WATANI USIKU:
JANUARI 1975
Yanga Vs Simba; Fainali, 2-0
WAFUNGAJI: Gibson Sembuli na Sunday Manara
Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati
JANUARI 1992
Simba Vs Yanga; Fainali
1-1, Simba ilishinda kwa penalti 5-4
Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati
JANUARI 12, 2011
Simba Vs Yanga; Fainali 2-0
WAFUNGAJI: Mussa Mgosi dk 33, Shijja Mkinna dk 71
(Uwanja wa Amaan, Zanzibar)
Kombe la Mapinduzi
OKTOBA 27, 1992
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Damian Morisho Kimti.
Ligi ya Muungano
AGOSTI 17, 2011
Simba vs Yanga 2-0, Dar
WAFUNGAJI:
Haruna Moshi ‘Boban’ dk 15 na Felix Sunzu dk 38.
Ngao ya Jamii
Comments