Lowassa Aongoza Harambee Ya Ujenzi Wa Kanisa La Moravian Ushirika Wa Mbezi Beach Jijini Dar
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akionyeshwa picha ya mfano wa Kanisa la Moravian Ushirika wa Mbezi Beach jijini Dar es Salaam na Askofu Mkuu wa Kanisa hilo Jimbo la Kusini,Askofu Lusekelo Mwakafwila kabla ya kuanza kwa Harambee ya Kuchangia ujenzi wa Kanisa hilo.Katika harambee hilo iliyoongozwa na Mh. Lowassa,jumla ya sh. Mil 70 zimechangishwa
Mwenyikiti wa Kamati ya Ujenzi wa Kanisa la Moravian Ushirika wa Mbezi Beach,George Nzunda akimpongeza Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa kwa kuendesha harambee ya Ujenzi wa Kanisa hilo iliyofanyika leo kanisani hapo.Katika harambee hiyo,Jumla ya shi. Mil. 70 zimepatikana ili kufanikisha ujenzi wa Kanisa hilo.
Hili ndilo Kanisa linalotakiwa kumalizika ujenzi wake ambalo harambee yake imefanyika leo na kuongozwa na Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa.
Picha na Othman Michuzi Jr
Phone: +255 (0) 713 775 869
Comments