Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akipokelewa katika uwanja wa ndege wa Zanzibar wakati akirejea kutoka nchini Marekani na Uingereza kwa ziara ya wiki mbili.(Picha, Salmin Said-Ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar
---
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad amerejea nchini leo tarehe 17/09/2012, baada ya kumaliza ziara yake ya wiki mbili nchini Marekani na Uingereza.

 Maalim Seif aliondoka nchini tarehe mosi mwezi huu kwa ajili ya kuhudhururia mkutano wa kimataifa unaohusiana na masuala ya demokrasia duniani, ulioandaliwa na taasisi ya National Democratic Institute katika mji wa North Carolina nchini Marekani. 

Baada ya kumaliza mkutano na makongamano yaliyoandaliwa na taasisi hiyo, Makamu wa Kwanza wa Rais aliendelea na ziara yake katika miji ya Washington na London ambako alikutana na kufanya mazungumzo na baadhi ya viongozi wa nchi hizo, pamoja na viongozi wa wa taasisi zinazoshughulikia sera za mahusiano ya kimataifa. 

Akiwa mjini Washington, Maalim Seif alikutana na msaidizi Waziri wa mambo ya nje wa Marekani anayeshughulikia masuala ya Afrika Bwana John Carlson katika jengo la Wizara hiyo mjini Washington, kuzungumzia juu hali ya maendeleo ya siasa na demokrasia Zanzibar. 

Pia alikutana na uongozi wa shirika la misaada la Marekani USAID, pamoja na kuzungumza na viongozi wa jumuiya ya wazanzibari wanaoishi nchini Marekani. 

Huko Uingereza Maalim Seif alikutana na mabalozi wa nchi za Afrika pamoja na maveterani wa Uingereza, ambao walikutana kuzungumzia masuala mbali mbali yanayohusu maendeleo ya Zanzibar tangu kuundwa kwa serikali ya Umoja wa kitaifa.
 
 Na 
Hassan Hamad
 Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar
 
 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA