MAKUNDI YA KIISLAM YADAIWA KUPANGA MAANDAMANO YA KUMNG’OA SHEIKH MKUU.
Sheikh Mkuu wa Tanzania Mufti Shaban Bin Simba
Na Datus Boniface.
Makundi ya waumini wa dini ya Kiislam wamepanga kufanya maandamano makubwa kwa lengo la kumng’oa Sheikh Mkuu wa Tanzania Mufti Shaban Bin Simba
Hatua hiyo inadaiwa kutokana na kutokuwa na imani na Mufti ambaye amekaa madarakani kwa muda mrefu huku Katiba ikimpa mamlaka ya kushika kiti hicho hadi pale atakapofariki.
Akizungumzia na waandishi wa habari katika ofisi za Bakwata, Ofisa Habari Shaban Simba, amekiri kupata taarifa hizo na kusema wamejipanga kukabiliana na lolote kutoka kwa kundi hilo la Waislam.
“Tumejipanga kukabiliana na hao wanataka kumn’goa kwa nguvu Mufti, lakini tunaomba jeshi la Polisi kuwadhbiti watu hawa” amesema.
Amesema wenye uwezo wa kumwondoa Mufti madarakani ni makubaliano maalum ya mabaraza mbalimbali ya kiislam yaliyoketi kujadili suala la kutokuwa na imani na Mufti na si vinginevyo.
Comments