Malema awashauri wanajeshi kudai haki zao

 
Mwanaharakati wa kisiasa nchini Afrika Kusini Julius Malema, amewashauri wanajeshi wenye manung'uniko kujipanga vyema na kupigania kazi zao.
 
Malema aliyatoa matamshi hayo kwa wanajeshi wanaokabiliwa na makosa ya kinidhamu yaliyotokana na maandamano waliyoyafanya mwaka 2009 wakidai mishahara mizuri na mazingira bora ya kazi.
 
Bwana Malema ni mwanasiasa anayeibua mgawanyiko hapa. Hivi maajuzi alifukuzwa kutoka chama cha ANC na kwa sasa anafanyiwa uchunguzi kuhusiana na kashfa ya ufisadi.

Lakini hajaondoka ANC kimya kimya. Badala yake ametumia mauaji ya hivi maajuzi katika mgodi wa Marikana kuanzisha kampeni kali dhidi ya mabepari nchini Afrika Kusini na kutaka yafanyike mapinduzi ya kiuchumi.

Wengi wanamshutumu kwa kuhusika na ubinafsi mbaya wa kisiasa, lakini malema anapokea uungwaji mkubwa kutoka kwa jamii za watu maskini na kimya cha serikali ni ishara tosha kuwa imeshindwa kukabiliana naye.

Manung'uniko ya wanajeshi ni fursa nyingine kwa Malema kuonyesha ubabe wake na hali ni tete nchini Afrika Kusini.

Hofu iliyopo ni kwamba migomo huenda ikaenea zaidi na kwamba serikali kwa sasa inazingirwa na migogoro ya ndani huku baadhi ya mirengo serikalini ikipanga njama ya kumtimua madarakani rais Jacob Zuma.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*