Mali mwenyeji wa kikosi cha pamoja

Serikali ya Mali imekubali kuwa mwenyeji wa jeshi la pamoja la nchi za kanda ya Afrika Magharibi ambalo litasiadia katika juhudi za kupambana na wapiganaji wa kiisilamu ambao wanadhibiti eneo la Kaskazini mwa nchi hiyo.
Nchi hiyo itatafuta uungwaji mkono wa umoja wa mataifa baadaye wiki hii kwa ushirikiano na muungano wa nchi za magharibi (Ecowas.)
Wanamgambo wa kiisilamu walitwaa eneo hilo mwezi Aprili na kusababisha hofu ya kuwepo vurugu katika kanda hiyo.
Awali Mali ilipinga kuwa mwenyeji wa kikosi hicho cha wanajeshi 3,000 mjini Bamako ingawa sasa imebadili msimamo wake.
Baada ya juhuzi kubwa za kidiplomasia zikijumuisha viongozi wa kanda hiyo, maafisa wakuu sasa wametoa idhini ya kuweza kuwa na kambi za jeshi hilo katika vitongoji vya mji mkuu.
Rais wa muda wa Mali, Dioncounda Traore alisemekana kutoridhia wanajeshi hao wageni kuwa nchini humo.
Wapiganaji hao wa kiisilamu walichukua udhibiti wa eneo la Kaskazini mwa nchi, baada ya nchi hiyo kukumbwa na vurugu kufuatia mapinduzi ya kijeshi yaliyofanyika mwezi Machi mapema mwaka huu.
Wapiganaji hao wameanza kutumia sheria za kiisilamu katika miji ya Timbuktu, Kidal na Gao huku madhabahu ya kale ambayo yanaonekana kama ambayo yanatumiwa kwa ushirikina yakiharibiwa.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*