Na
Anna Nkinda – Maelezo
21/9/2012 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete
amewataka wanafunzi wa kike nchini kutochanganya mapenzi na shule kwa wakati
mmoja kwani kwa kufanya hivyo wanaweza kupata maambukizo ya Virusi
vinavyosababisha ugonjwa wa Ukimwi pamoja na ujauzito na hivyo
kutotimiza ndoto zao katika maisha yao ya baadaye.
Mama
Kikwete ambaye pia ni mlezi wa shule ya Sekondari ya wasichana ya Mandera
iliyopo Bagamoyo mkoani Pwani aliyasema hayo jana wakati alipotembelea shule
hiyo kwa ajili ya kuwatakia heri wanafunzi wa kidato cha nne wanaotarajia kuanza
mitihani yao ya mwisho mapema mwezi ujao.
Aliwataka
wanafunzi kutumia muda wao wa masomo kwa manufaa ikiwa ni pamoja na kusoma kwa
bidii kwani itawasaidia katika maisha yao ya baadaye na kuwa
wataalamu wazuri katika nchi yao.
“Jiepusheni
na mazingira yatakayowapelekea kupata ujauzito na kukatisha masomo yenu kwani
mimba ni adui wa maendeleoa ya msichana, inatia uchungu kuona
mwanafunzi anapata ujauzito lazima mjitambue kuwa
ninyi ni wa thamani mnatakiwa kujitunza”, alisema Mama Kikwete.
Kuhusiana
na maambukizi ya Ugonjwa wa Ukimwi Mama Kikwete alisema kuwa hivi sasa
watu wengi wamekuwa na tabia ya kuwa na mpenzi zaidi ya mmoja na
kama mmoja wao atakuwa amepata maambukizi ni rahisi kuwaambukiza
wote aliopo katika mtandao huo wa mapenzi.
Mlezi
huyo wa shule aliwaasa wanafunzi hao kuridhika na vitu wanavyopewa na wazazi wao
hata kama ni vidogo lakini kama hawataridhika na kutaka kupata vitu vingi vyenye
thamani kwa njia ya mkato matokeo yake ni kupata ujauzito na ugonjwa wa Ukimwi.
.
Akisoma
taarifa ya shule hiyo Mkuu wa Shule Rose Umila alisema kuwa mahudhurio ya baadhi
ya wanafunzi yamekuwa siyo mazuri kutokana na baadhi ya wazazi kuwa na uelewa
mdogo juu ya kuwaelimisha watoto wa kike na baadhi yao kutowasomesha watoto wa
kike kwa madai ya kipato duni hali inadhorotesha maendeleo ya mtoto wa kike.
Umila
alizitaja changamoto wanazokabiliana nazo kuwa ni pamoja na
upungufu wa vyumba vya madarasa vitano, maabara tatu, maktaba
moja, mabweni manne, bwalo moja na matundu ya vyoo ishirini,
mabafu 12, stoo moja, nyumba za walimu 20 na jengo la utawala
moja.
Kwa
upande wa thamani shule hiyo inaupungufu wa meza 361, viti 259, meza za walimu
tano, na viti vya walimu vitano hata hivyo kwa kushirikiana na
wazazi shule hiyo imeweza kutengeneza meza na madawati 50, meza saba na
maabara.
Shule
ya Sekondari ya wasichana Mandera ambayo kwa mwaka huu itatoa
wanafunzi wa kidato cha nne kwa mara ya kwanza inawanafunzi 590 ambao kidato cha
kwanza ni 120, cha pili 121, cha tatu 181 na cha nne 178 na walimu
12 kati yao wa masomo ya sanaa tisa na sayansi watatu.
Mwisho.
|
MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA
1. Wahiraki, Hawa ni wanawake wa jamii ya Wahiraki wa napatikana kaskazini mwa Tanzania wamezagaa mikoa ya manyara ni weupe Wana Umbo zuri wanavutia kwa Macho. 2. Warangi, Hawa ni wanawake jamii ya Warangi ni wazuri nywele zao ni asili ya waraabu weupe sura nzuri wanapatikana kondoa. 3. Wanyiramba. Hawa ni warembo Sana sura matata wanapatikana mkoa wa singida kaskazini, usipokua makini utawafananisha na wanyaturu 4. Wamasai, kabila hili wanawake wazuri sio wengi Sana lakini ukikutana na sampuli Tatu au nne hivi utauza hata boxa kuongezea mahari wamezagaa Sana Arusha 5. Wahaya, hawa nao ni jamii ya Kanda ya ziwa maumbile Yao Kuna weupe miguu Yao ya bia shape matata wamejaa Sana bukoba. 6. Wanyaturu, Hawa wanafanana na Wanyiramba wanapatikana singida hasa ikungi na manyoni weupe wanavutia 7. Wapare, Hii ni jamii ya kabila la Wapare wanapatikana moshi wilaya ya same wako vizuri usicheze kabisa na hili kabila shape nzuri. 8 .Wamakonde, Hawa wanapatikana kusini mwa Tanzania ni kab
Comments